KATOTO KA FORM ONE πŸ”ž (22)

SEHEMU YA 22
Bila kuongea chochote, Nurat alitoka mbio kuelekea chumbani huku moyo ukimdunda sana.

β€œMungu wangu!!! Ndo nimefanya nini?” aliongea kwa hasira na aibu β€œMimi nilijua yupo Ommy jamani kaaah!” alizidi kusema huku akiwa ameweka viganja vyake mdomoni kwa aibu β€œSasa atanionaje?” aliwaza

Wakati anawaza hayo, pia Baba Denis naye alikuwa akiwaza yake β€œHuyu ntoto ni shetani au?” alijisemea huku akiwa emeshika tama β€œKwanini anafanya hivi huku ndani? Au anampenda Omary? Hapa lazima kuna siri” alitafakari kisha akainuka ili aende chumbani kukaa na mkewe

Ghafla kabla hajaondoka alisikia hatua zikija sebuleni, akageuka na kukuta Winnie. Alipomaliza aligeuza shingo na kuendelea na safari yake lakini hakufika mbali akapata wazo na kumuita
β€œWinifrida” alisema mzee huyo

β€œAbee” Binti alisema huku akiibinya midomo kwa ndani na kufanya mashavu yabonyee β€œShikamoo baba”

β€œMarahaba, samahani kwanini huendagi ibadani?”

β€œAam….mh aah” alianza kupata kigugumizi ndipo mzee akajikoholesha.

β€œAnyway, unaonekana hauna sababu ya msingi ila jitahidi uwe unahudhuria” alisema mzee huyo

β€œSawa baba”

β€œSamahani kuna kitu nataka unieleze kwa kina” alisema Mzee

β€œKitu gani baba?” aliuliza

Mzee alishusha sauti na kuweza kuongea bila mtu mwingine kusikia
β€œHivi Nurat na Omary wana mahusiano gani?” aliuliza

β€œHeeeh” Winnie alishangaa na kushika kiuno halafu akacheka kwa nguvu

β€œSsssh” mzee alimzima β€œTumia sauti ndogo”

Sasa kumbuka Winnie ana bifu na Nurat hivyo aliitumia ile fursa vizuri
β€œSawa, acha nikueleze…..huyu Nurat muda mrefu yuko katika Mahusiano na Ommy…..mbaya zaidi pia yuko na Denis, anawachanganya” aliamua kumwaga mchele

β€œJesus!!!” Mzee alishtuka

β€œNdio hivyo, hapa hatoweza kufaulu kwani kwanza ana simu kubwa nimekuta akiwatumia picha za uchi wanaume mtandaoni?”

β€œWinifrida……are you serious?”

β€œYes”

β€œKwanini hukusema?”

β€œSikupata nafasi ya kusema” alisema na kuondoka zake, lakini alimuacha mzee mdomo wazi anashangaa

Mzee alipagawa ikabidi aende chumbani kujadili na mkewe…..JE ITAKUWAJE? WATAMNYANG’ANYA SIMU?
USIKOSE

Share kwa ndugu na marafiki

WhatsApp
Facebook
Twitter

Chagua kipande kinachofuata

error: Content is protected !!