SEASON 4: BINTI MDUNGUAJI (60)

SEHEMU YA SITINI

ILIPOISHIA SEHEMU YA HAMSINI NA TISA : kama livyo tegemea, akamwona yule kaka wa bandia akijitokeza mbele yake, na kusimama akiwa na bisi bisi mkononi, “sikia we mwanamke, kimya kimya, ukipiga kelele nakutoboa, chakufanya vuanguo zako zote, mpaka hiyo bangiri, viatu na hizo hizo eleni na cheni” aliongea Mchafu, kwasauti yachini, huku akianza kulegeza mkanda wa suluali yake, kwa mkono mmoja, humu mkono mwangine bado ameshikilia ile bisi bisi, “sasa kaka mbona unavua suluali” endelea ……..
Aliongea Jackline kwa sauti ambayo ilimshangaza Mbwa Mchafu, maana aikuwa na atachembe ya uoga, mchafu akainua macho kumtazama Jackline, ambae kiukweli umbo lake na uzuri wake, alionekana kuwa mwanamke wa kaida tena mrembo sana, akuwa polisi na wala asingeweza kujitetea mbele yake, “unauliza jibu, siwezi kukuacha mrembo kama wewe” aliongea Mchafu huku akiendelea kulegeza suluali yake, “unazani nilahisi hivyo” aliuliza Jackline akiwa amesimama pale pale mlangoni, (siyo wakutokea nje kabisa) “ujasikia nilicho kuambia we kenge, ebu vua kila kitu” aliongea tena mchafu safari hii kwa suti yachini lakini ilitawaliwa na ukari, “kaka nazani siku yako ime fika, maana siutarajia kuuwa tena hivi karibuni, lakini wewe sikuachi salama” aliongea Jackline na kumshangaza yule kijana, ambae aliinua macho yake na kumtazama mwamke huyu, “unajifanya una ……” mbwa mchafu akuwai kumalizia maneno yake alishangaa ghafla yule mwanamke mrembo akinyoosha mono wake, kama umeme akaichomoa ile bisi bisi mikononi mwake, mpaka hapo mbwa mchafu alianza kuhisi kuwa aliepo mbele yake siyo mwanamke wa kawaida, akamtumbulia macho akimshangaa “karibu kuzimu” alionge Jackline huku anaishindilia ile bisi bisi shingoni kwa Mbwa mchafu kisha aka mshika na kumvutia ndani ya choo, na kumsukumia kwenye sink, kama kiroba, Mbwa Mchafu akajibwaga akitanguliza uso uliotuwa kwenye sink la choo, uku akiushindilia msumali wa ile bisi bisi, ukijishindilia shingoni kwa mbwa Machafu nakuja kutokea nyuma yashingo karibu kidogo na kisogo, kisha Jackine akaufunga mlango wa kile choo kwa nje, alafu akanawa mikono yake kwenye sink la kunawia, kisha akatoa nje ya choo, Jakline alimwona yule kijana msimamizi wa vyoo, ambae alistuka sana alipo mwona akitoka chooni, huku yule kijana akiwa amezungukwa na wanawake watatu, “we siumesema kuna fundi huko ndani, mbona huyu dada ametona huko huko” aliuliza kwa kulalamika mmoja kati ya wale wanawake, ambapo Jackline alipita pale alipokaa yule kijana huku akimwambia, “aijawa kuwa lahisi” Jakline akusubiri jibu ambalo lilionekana wazi kuwa, lisinge toka hivi karibuni, akatembea zake kuelekea ndani ya ukumbi wa canteen, akipanga kwenda kumdanganya Denis kuwa anaumwa waondoke mala moja, tena alipanga kumtajia ugonjwa ambao lazima wangeinuka mala moja, ** baada ya kuiona sura ya mwanamke mrembo ambae alikuwa ngeni kwake, Pc Busungu akiwa kama wanaume wengine wenye afya njema ya uzazi akajikuta akipata tamaa ya kuongea na yule mwanamke, ambae alikuwa na uakikakuwa anarudi, baada ya kutokea mlango wa uani, ambako akukuwa na njia ya kutokea moja kwa moja, nje ya canteen, akiwa bado anakumbuka wapi alipomwona huyu dada, pengine angepata njia ya kuanzia kuongea nae, mala akamwona yule dada akiingia, akamtazama tena “yani ile sura inanjia kabisa, sijuwi nimewai kumwona wapi?” aliwaza Busungu, wakati huo yule dada nae, alimtazama Busungu na macho yao yaka gongana, lakini akuonyesha kumfahamu yeye, “itakuwa nafahamiana nae lakini amenisahau” aliwaza Busungu huku akiendelea kumtazama yule dada ambae aliekea moja kwa moja mpaka kwenye meza moja iliyokuwa imekaliwa na jamaa moja na mtoto mdogo sana aliekalishwa kwenye kiti, yule dada akukaa akaonekana akimnong’oneza jambo yule jamaa ambae alionekana kuwa mumewake, wakaonekana kujadiri kidogo, kisha akamwona yule jamaa akisimama, na kumnyanyua yule mtoto mdogo, kisha yule mwanamke akachukuwa mkoba wake, kisha wakatembea kutoka nje, ya canteen, nakupotelea nje kabisa, “lakini mbona kama nimeshawa kumwona” alijiuliza Busungu, wakati huo huo zikasikika kelele kutoka nje ya canteen upande wa vyooni, “jamani kunamtu amekufaaa” sauti hizo za mayowe zilitoka kwa wakina mama na kijana mtuza choo, “Mbwa mchafu, amekufa hukuuuuuuuuu” kelele zilikuwa nyingi sana, Pc Busungu alikuwa mmoja wawatu walio simama haraka na kumbilia chooni, akiongozana na polisi waliovalia sale za kazi, waliokuwa wanapata chakula, ambako waliingia kwenye choo cha wanawake, na kumkuta kijana yule akiwa ameingiza kichwa kwenye sink la choo, huku msumari wa bisibisi, ukitokeza nyuma ya shingo, “daah! imekuwaje tena huku choo cha kike Mbwa Mchamfu” aliongea mmoja wapolisi, kwa sauti ya kunong’ona, ambayo ilimfikia busungu, ambae alionekana ku gundua kitu, “yupo wapi msimamizi wa vyoo” aliuliza Busungu huku akitoka nje ya choo, akiwaacha wenzie wanapiga simu kituo kikuu, akamkuta yule kijana msimamizi wa vyoo akiwa ameshikiliwa na polisi wawili, akionekana amechanganyikiwa, “we! ebu eleza, nani meuwa?” aliuliza kwa ukari Pc Busungu, “afande siyo mimi, Mchafu mwenyewe alitaka kumwibia huyo dada” alisema yule jamaa, ambae mpaka hapo kama wange mkagua, wangekuta amesha jisaidia haja zote, “yupo wapi huyo mwanamke, na ilikuwaje?” aliuliza Busungu, akimtikisa tikisa kijana mtunza vyoo, “Mchafu alinitisha kisha akaimfwata yule dada chooni, mala yule dada akatoka, akaniambia kuwa ‘aijawai kuwa lahisi” alimaliza kueleza kijana yule, ambae mpaka sasa miguu ilikuwa ina mtetemeka, hapo Busungu akavuta kumbu kumbu ya mwisho kuyasikia maneno yale, “Jackline Nyati” alinongo’ona Busungu baada ya kukumbuka maneno yale ambayo aliyasikia Songea, miezi tisa iliyopita, kwa mzee Nyati, Busungu alitoa simu yake mfukoni, huku ana chomoka kuelekea nje ya jengo la canteen, nakufwata uelekeo ambao alielekea yule mwanamke na mume wake, ambae Busungu kwa sasa alikuwa na uakika ni Jackline Nyati, ambae aliwai kumwona mwaka mmoja na miezi sita iliyo pita, na kiuakika alikuwa amemkumbuka kabisa kuwa ni yeye, Busungu alipiga simu kwa insp Johnson, akamweleza juu ya tukio hilo, la kuuwawa kwa kibaka mzoefu, na alikuwa anamshuku Jackline Nyati kuusika na tukio hilo, kwa hiyo muuwajai yupo eneo hili la kaliakoo, ** Jackline na Denis walikuwa na mtoto wao, walikuwa ndani ya gari wakijiandaa kuondoka, mala Jackline akamwona insp Johnson akiwa na kundi la askari, wakitokea kituo kiuu wana kuja uswa wao huku akiwaonyesha ishala askari wake kuzunguka eneo lile, “hivi Denis, mbona unachelwa jamani, si nimekuambia mwezio najisikia vibaya lakini” aliongea Jackline kwa sauti ya kiunyonge ambayo ili mfanya Denis awashe gari na kuanza kuondoa gari taratibu, toka kwenye kituo cha mafuta na kushika njia ya uelekea fire, Jackline akageuka na kutazama walikotoka akamwona insp Johnson akiwa anaendelea kuwapanga Askari wake, wao wakaondoka na kutokomea, wakiikamata barabara ya morogoro, ** insp Johnson akiwa na uakika kuwa Jackline atakuwa na ile gari Toyota lav 4 akaagiza kuzuiwa kwa gari kama hizo huku wakitoa taalifa njia zote za jiji la dar kuzuwia gari za aina hiyo, kisha yeye akaelekea canteen ambako alikutana na pc Busungu, ambae alimsiulia jinsi alivyo mwona yule mwanamke na kushindwa kumkumbuka, taratibu za kuupeleka mwili wa marehemu Mbwa Mchafu muhimbili zilifanyika, huku yule msimamizi wa vyoo akipelekwa kituoni kwa mahojiano zaidi, taalifa za mauwaji ya Mbwa mchafu zilitapakaa kama moto wa petorol, nusu saa baadae ata vyombo vya habari vilishaanza kutangaza, juu ya tukio hilo, kila chombo cha habari kikisimuila kwanamna ilivyo juwa, wakati wengine wakilahani vikali juu ya mauwaji hayo lakini walioona mbali walifanya uchambuzi juu ya matukio ya muuwaji kuwauwa waalifu, kiukweli tukio hili lili mpa wakati mgumu sana insp Johnson, ambae alikuwa anaona kila dalili ya muuwaji Jackline, kujitengenezea sifa kwa wananchi, hivyo ingempa wakati mgumu kuzuwia mauwaji ya baba yake, ambae nayeye atabainika kuwa ni mwalifu, kama waalifu wengine watakao uwawa na walio huwawa, “kuna kila sababu ya kumsaka huyu malaya, na kumchinja kimya kimya” aliongea Johnson akimwambia Busungu, “tena inabidi tucheze sana kuanzia mbezi mpaka kibamba” aliongea tena Johnson, “unajuwa nini afande, kitu kinacho ni furahisha nikwamba, yule mwanamke anikumbuki kabisa” aliongea Busungu kwa kujiamini, “busungu, kunakitu nimejifunza, huyu awa watu wana akili zaidi ya watu mia hamsini, unaweza kuzani ajakufahamu kumbe alisha kuona mda mrefu sana” aliongea insp Johnson ambae kiukweli alisha waogopa sana watu anao watafuta, “ila afande akuonyesha dalili yoyote ya kustuka wala kunitambua” aliongea Busungu akionyeshe kuwa na uakika zaidi, “ok! jukumu la kibambanitakuachia wewe, ila itabidi tutafute askari wa nne watakao mfatilia mzee Masinde, na kuakikisha usalama wake bila yeye mwenyewe kujuwa” ** Mazao Building ndani ya ofisi ya kina mahadhi palionekana watu zaidi ya sita, wakijadili jambo flani, pamoja na wakina Mahadhi boss na Janet, walikuwepo wanaume wegine wawili, mmoja kiwa mwenye hasiri ya kihindi, na mwingine mtanzania, pia alikuwepo mwanamke mtanzania, walionekana kujadiliana jambo flani, ambalo lilitakiwa lifanyike kwa siri pasipo Denis kufahamu, “yani Mahadhi ata kwabhati mbaya usije kumwambia, maana akijuwa tumesha vuruga kila kitu” alisisitiza boss wao, “kwani mimi ndio mbeya sana?” aliuliza Mahadhi kwa mshangao, “tena alivyo kuwa rafiki yako, sijuwi kama utavumilia usimwambie” aliongea Janet, “nazani tumesha maliza, chamsingi ngoja tupelekea jibu, alafu tutawasiliana” alisema yule mwnye hasiri ya kihindi, kisha akaondoka na wale wenzie mwanamke na mwanamume, *** saa tisa jioni Deni na familia yake ndio walikuwa wanakatiza mbezi, akiwa wamesha poteza mda mwingi sana pale kimara walip kuwa wanapata chakula baada ya kushindwa kula Kaliakoo, “unajuwa wewe nikama unamajini” aliongea Denis wakati wakiwa wanaingia mbezi, kauli hiyo ilimtisha sana Jackline akamtazama Denis, “kwanini?” aliuliza Jackline kwa mashangao, “yani unamachele mpaka nakuogopa, unajuwa pale tulipoondoka ndipo palipo tokea mauwaji, tuliyo ona yanatangazwa pale kwenye TV pale kimara?” aliongea Denis, akiwa anaendasha gari taratibu, kutokana na msongamano wa gari, ya pale mbezi mwisho, “he! unasema kweli? kumbe ni pale tulipotokea sisi” alijifanya kushangaa Jackline, huku moyoni akipata afuweni, maana alizan kuw Denis amemstukia, “yani imenishangaza sana, tena nichoo kile kile ulicho enda wewe” aliongea Denis, na wakati huo huo akasikia simu yake ikiita, akaitazama ilikuwa namba ngeni, akaipokea huku anaendesha gari taratibu, akaanza kuongea pasipo upande wapili kusikika, “ndio naitwa Denis,…… ndio… nipo mbezi, naenda nyumbani ….. inahusu nini?………. lakini kwanini usije ofidin jumatatu?….. yani nipo na familia alafu nimechoka sana, ……. ok! jitaidi basi niwai nikapumzike, nakusubiri hapa full dose” aliongea Denis na kukata kona kuingia barabara ya zamani, kisha akaegesha gari kwenye maegesho ya Full Dose Pub, ambayo mmwaka mmoja na miezi kama sita iliyopita palitokea mauwaji yakutisha ya watu wawili, akiwemo polisi, “vipi baba France, kuna nini?” aliuliza Jackline akiwa ameingiwa na wasi wasi kidogo, “kuna mtu anasema kuwa anainshu muhimu ya kuniambia, hivyo tumsubiri hapa” hapo kengere ya hatari ikagonga kichwani kwa Jackline, “unauakika kuwa huyo mtu ni mzuri kwetu?” aliuliza Jackline wakati wakiingia ndani ya Pub, Denis akiwa amembeba Fransis, “punguza wasi wasi, mke wangu, sizani kama kuna tatizo, sababu sina maadui” alijibu Denis kwa sauti flani ya kumpooza mke wake, walikaa kwenye meza moja, aliyo ichagua Jackline, iliyo kuwa kwenye kona kabisa ya ukumbi wa ile Pub, ambayo kwa sasa ndio ilikuwa inaanza kupata wateja baada ya mda mrefu kupita, toka mauwaji yatokee, “maadui wabaya zaidi ni wale wasiri” aliongea Jackline au mama France, wakati huo mhudumu alikuja kuwa sikiliza, wakaagiza vinywaji kilammoja anacho kipenda, wakati Jackline akiagiza soda Denis aliagiza bia, “wala usiwe na wasi wasi mke wangu nazani ni mambo ya kiofisi tu!” alisema Denis wakati mmuhudumu ameenda kuwa letea vinywaji, hapo Jackline akatulia na kuanza kulisoma eneo lote la bar, ata vinywaji vilipo fika waliendelea kunywwa wakiongea hili na hili, lakini Jackline aliendelea kusoma eneo, na kwamba atatokaje, endapo ikitokea wanae mmsubiri ni polisi, japo ilikuwa nilazima asubiri, kusikiliza hicho alicho taka kuongea huyo mtu asie fahamika, mda ulienda masaa yaka katika giza likaanza kuingia, huku mala kwa mala Denis akionekana kupiga simu kwa mtu wanae msubiri, mwanzo alikuwa anapokea na kusema yupo njiani, lakini kila mda ulipozidi kuyoyoma, ndipo Denis alipo piga simu pasipo mafanikio, maana simu aikupokelewa, Denis alisha kunywa pombe nyingi sana, kiasi cha kuanza kulewa sana, “twende nyumbani nisije kushindwa kuendesha gari” alisema Denis, kisha wakainuka na kuondoka zao, huku Jackline akijitaidi kuwa makini sana maana alihisi kuwa kuna kitu kinaweza kutokea mda wowote, saa moja nanusu safari ilianza kuelekea nyumbani kwao kibamba, huku giza likiwa limesha tanda, maongezi yalikuwa mengi wakikumbushana siku za nyuma, asa siku ile walipokutana kwa mala yakwanza, walicheka sana, lakini wakatu huo Jackline alikuwa ana mfwatilia mtu mmoja aliekuwa akiwafwata kwanyuma na pikipiki toka wakiwa wanatoka mbezi, mpaka wanafika kibamba njia panda, na kukata kulia kuelekea kwao, na yule jmaa alie valia koti jeusi na kofiangumu ya kuendeshea pikipiki na yeye alikata kona kuwa fwata, hapo Jackline akatabasamu kidogo, “hivi nyumbani unabia kweli?” aliuliza Jackline, “zipo nyingi sana, vipi unataka kunywa” aliongea Denis wakati wana karibia kukata kona kuingia kwao kabisa, “labda unge nunua wine, lakini bia siwezi” alijibu Jackline huku anageuka kutazama mwendesha piki piki aliekuwa anawafata, alimwona bado anawafwata, Jackline akatazama mbele ilipo nyumba yao, akaiona inawaka taa, za nje na za ndani, “mh! baba France nikweli atukuzima taa zote?” aliuliza Jackline akitazama nyumba yao kwa umakini sana, mbapo aligundua uwepo wa mtu ndani ya nyumba hile, kwa kuona kumvuli kwenye mapanzia, “inaawwezekana ila…ila..” aliongea Denis huku akizidi kuisogelea nyumba na kusimamisha gari, kwenye uwanja wanyumba yake, Jackline akamwona yule mwendesha pikipiki, akiwa amesimamisha pikipiki kwa mbai akitazama upande wao, “sikia baba France, ebu nipe funguo ya nyumba, wewe na mtoto subirini kwenye gari, nikafungue kwanza mlango” aliongea Jackline, baada ya kuona kuwa mume wake akuwa na wasi wasi wowote, juu ya kinacho endelea, labda kutokana na pombe alizo kunywa, hapo Denis akaanza kujipekua kutafuta fungu, lakini akuipata ata kidogo, aliangaika sana lakini akuipata, “sijuwi nimeiweka wapi?” alijiuliza Denis, na Jackline akawa amesha hisi kitu, akashuka toka kwenye gari, akatembea kawaida tu! akijifanya kuwatokuwa na tahadhari yoyote, lakini ile anaufikia mlango, na kujaribu kufungua mlango, taa zote zikazima kwa pamoja, kama vile umeme umekatika, huku mlango ukifunguka, “kumekucha” aliongea Eva akijibanza pembeni ya mlango akiwaza namna ya kufanya tukio bila Denis kuona, nyumba nyingine zote zilikuwa na umeme, kasolo yakwao tu, Jackline akatuliza akili akasikiliza kwa umakini, akasikia michacho ya nyayo za watu toka ndani, hapo Jackline akaona bola aingie ndani akawamalize huko huko, pasipo Denis kuona, lakini kabla ajapiga hatua kuingia ndani

Share kwa ndugu na marafiki

WhatsApp
Facebook
Twitter

Chagua kipande kinachofuata