CONNECTION YA BALTASAR (12)

SEHEMU YA 12
  
Hivi ushawahi kukataliwa wewee?? Yaan mwanaume amekunyandua halafu anakukatia hapo hapo bila hata chenga haulizi wala hakwepesh yaan ile No kukupa matumainiii

   Kwanza nilihisi utani mana mussa kwa hizi siku nilizomjua alikuwa mtu wa utani utani sanaaa

Kwahiyo mie nikachukulia hivyo hivyo kwamba ni mtu wa utani na hapo ananitania

Nikasema  mussa acha utani !!” Huku najikaliza vizuri kwenye kochi

  Akanambia  Yeah I’m Serious  siwezi kukupa moyo Dina wala siwezi kuoa

🙄🙄mungu wanguuuuu🙆‍♀️🙆‍♀️🙆‍♀️na nilisema swala la kuoa wala sikua namaanisha unajua ni kama nililopoka tu sikutegemea kukutana na haya majibu

“Dinna  unajua Umeni surprise sana ,sikutegemea kama naweza kukuta ukiwa hivyo ,yaan nashindwa hata niseme nini but sorry sana Dinna “

Uwiii😭😭😭Nikamuona huyu kaka kichaa ndio nikaanza kulia sasa ile ya Serious mana mwanzo nilikuwa nalia kwa kudeka hee kumbe hakuna mtu wa kumdekea hivyooo😭😭😭

  “We kaka weweeee aah””

“Sorry Di..” nilimuweka bonge wa kibao nikainuka haraka nikatoka nje nakimbia akawa ananiita mie nikafungua geti nae akatoka mbio ananiita Dina njoo tuongee sikusimama hata nikachukua Boda mbele nikamwambia nipeleke kituoni 

Nimefika kituoni na gari inafika nikapanda yaan nimekuja kukumbuka yule kaka sikumpa hata hela ya boda atajua yeyeee😭😭

Kondaa kaja kudai nauli sina hata mia wacha niangue kilio cha nguvu abilia wote wananishangaa mimi tu  mmoja akaniambia njoo ukae hapa yeye akainuk mana mie nilikuwa nimesimama

Konda hakuniuliza tena hata nauli ,sasa zile foleni za kutoka mbezi nimefika kwetu giza limekorea kweli kweli

Ile nashuka kwenye dala dala ndio najikuta nipo peku sasaa😫😫😫😫kumbe hata viatu niliacha kwa mussa jamani
Simu sinaa 😭😭walai nimevurugwa miee daaah

  Nilifika nyumbani  nikamkuta mama anaangalia Tamthilia zake

“We nae ndo unanirudia sa hizi,pamekuwa kwako hapa et??”

Maneno ya mama yalikuwa kama mkuki moyoni mwanguu😭😭😭🙏 eeh mungu wee nililia kwa sautii mama akabaki ananitazama kwa mshangao

  Nilienda nikapiga magoti mbele yake

🙏🙏 “mama yangu mamayangu  nimekosa mie mama yangu ,walau ningekusikiliza kidogo tu mama kidogo tuuu labda nngekuwa na heshima yanguu , ulinambia mama mwanaume anakupenda akiwa hajapata anachotak kwenye nguo zako akipata tu anakuona kama paka ,Mama yule mwanaume ameniona mie mbwa mamaaa😭😭 mama niuwe kabisa mama yangu we niuwe tu “

“Embu nyamaza halafu ongea vizuri unanichanganya mjinga wewe”
Mama aliongea kwa kufoka lakini sauti yake ilikuwa  na wasi wasi mwingiii wenye Hofuu

Mie ndio nakazana kulia sanaa yaan yale majuto yananikaba kwenye koo mpaka basii najuta najuta najutaa

  Mama akanituliza kwanza sikuwa na mtu wa kumlilia nilimuhadithia mama yotee kama kunipiga acha anipige ili akili inikae sawa

Nikamwambia  mama umenifunza vyema sana lakini mie nimekataa sasa naona ulimwengu umenifunza kwa ukali naumia mama nilimpenda yule mwanaume bila hata kumjua vizuri  mamaaa
  
Mama akanambia  tulia  Dinaa mwanangu tulia mwache na inshaallah  utapata aliesahihi muda sio mrefu achaa  chochote kinachotokea mungu ndio kapanga yeye kakuumiza basi amini ataumia zaidi yako hata kama usipo muona lakini ataumia kuliko hata wewe “

Nikamwambia mbona haunipiga mamaa na nimevunja usichana ulio ulinda kwa nguvu zote??😭😭

Akanambia  haina hajaa hata hivyo  umejitunza sana mtoto wangu  upo tofauti sana na ma bint wa mtaani  hufanani tabia na watoto wa wanawake wenzangu wengi najivunia wewe , umeshaona kile nilichokuwa naulindia sio usichana bali sikutaka uchezewe sikutaka uumie kisa mwanaume  lakini nimeshindwa na umeumizwa tena mara ya kwanza tu , sasa kuanzia hapa Jilinde mwenyewe  kuanzia hapa jitunze mwenyewe  huwezi kulazimisha moyo wa mtu ukupende hata tukitumia nguvu utaumia zaidi huko mbele

Kaa tulia utapata aliesahihi kwa wakati sahihi  na utafurahia mahusiano  kamwe usijitoe kama njungu mtaani kisa tu kukataliwa na mbwa mmoja sawaa”

‘”Asante mama yangu Asante “😭🙏

“Hayaa kaoge uje ulee , ulale sitaki tena ulie wala umkumbuke huyo mpumbavu”

“Sawa mama”

Niliinuka nikaenda kuoga lakini swala la kumsahau mussa aisee lilikuwa gumu sanaa yule mtu nilikuwa nimeshampenda sanaa yaan nimezama mwili na moyo ,figo mpaka maini kutoa kutoa vyote ndio na mie nitoke sio haraka hivyo aisee

Bafuni nililia sanaa mpaka mafuaa, mama alipoona nimeingia moja kwa moja akaja akaniita nikafuta machozi nikatoka sikuwa na hamu ya kula ,

Nyie mapenzi kumbe ndio yanauma hivii yaan kama kuna donda kubwaaa kati kati ya moyo kila ukipiga Du Du Du ,ndio unaenda kutonesha lile donda maumivu makali nayasikia 

Nikamwambia mie naenda kulala nimeshiba akanambia sawa wala hakunilazimisha kula akanambia  kama unasikia uchungu lia sanaa sintakuzuia ila iwe leo tu hakikisha usiku wa leo ndio mwisho wa kumlilia mpuuzi ambae yeye huko alipo anafurahia wakati wewe unauma

Nikasema sawa mama😭😭 nikaingi kulala jamni nyieee🙌😔😔 Usingizi hauji nalia mbona mie mzurii tena sanaa tu sasa mbona mussa amenifanya hiviii au kwakua anahelaa au amenionaje miee
  Nilitamani hata kumpigia labda niongee nae lakini simu nayo nimeacha huko huko kwake

Nilikuwa nakumbuka yale mapenzi the way alivyokuwa nananipapasa kwa mahaba mazito zile sifa alikuwa ananimwagia ile miguno yake 🙌🙌🙌mamaee kumbe alikuwa ananiigiziaaa

Share kwa ndugu na marafiki

WhatsApp
Facebook
Twitter

Chagua kipande kinachofuata