CONNECTION YA BALTASAR (19)

SEHEMU YA 19

 Akanivuta akawa amenikumbatia akanambia  naomba tuongee mke Wang”

Nikamwambia acha kuniigizia wewe!!

“Noo Mamyyy mie mbona sikuigiziii”

“Utajua wewe!!”

Alinivuta kwa nguvu akanikumbatia kwa nguvuuuu akanambia  Dina kweli ukweli  nilikupenda tangu nilipo kuona kule fb ile siku   nilikupenda lakini sikujua kama tutafika huku”

Yaan huyuuu😫😫 enhee alijua tutaishia wapiii si ndio mie nasema hanipendi huyu kaka huyuuu

“Embu nisikilize Dina naomba unisamehe mama yangu nakuombaa , najua halikuhusu lakini naomba nikuambie hili lililofanya mie nisiwatamani wanawake kuwaweka karibu yangu walau nisikilize tuuu nilitoe la moyoni “

“Enhee nakusikia”

“Keti basiii” nilivuta kiti kwa hasira kwali nikaketi

“Unajua mie nilishawahi kuwa na mke hapo zamani nikajaariwa mtoto mmoja , mtoto wangu alikuwa ndio kila kitu  nilimuweka mbele kwa kila kitu mke wangu nilimpenda sana, lakini unajua alikuja kufanya ninii??”

Nilitikisa Kichwa kuwa sijui alifanya nini!!

“Yule mwanamke  alikuwa na kaka yake ambae alimuombea kazi kwangu , alikuwa shemeji yangu, nilimpatia usimamizi kwenye kitengo flani kwenye kampuni wala hakuwa na uzoefu wala elimu lakini ni shemeji nilimpa nafasi

  Shemeji  yangu nilimpa nyumba ya kuishi baada ya mke wangu kumuombea sehemu ya kukaa ,  

Ndie mtu aliekuwa karibu mnoo na mke wangu karibu  kuliko kawaida nilikuwa nikisafiri kaka yake anakuja nyumbani pale kukaa mpaka nitakapo rudi ndie nae anaondoka
Mke wangu alikuwa anasema  kukaa peke yake kwenye nyumba  kubwa anaogopa ..
.  Alishika ujauzito  akajifungua mtoto wetu wa kwanza alifanana kila kitu na kaka yake kila kituuu
 
Mtoto alivyofika miaka minne ndio nilianza kuona mambo ya ajabu mke wangu na kaka yake  walikuwa wakigombana sana kuhusu mtoto sanaa

Mda wote kaka yake alikuwa anamchukua mtoto anavyojisikia kitu ambacho mke wangu alikuwa hapendi sana

Mwenyewe  nilikuwa namwambia embu mwache mtu na Uncle wake tu hao  wanapendanaa


Siku moja nilikuwa natoka safari nilikuta ugomvi nyumbani  mkubwa sana shemu akawa anamwambia dada yake mwambie ukweli mumeo kama ukishindwa mie nitasema

Hawakuwa wanajua kama nimefika niliuliza ukweli gani??

Dada yake akaanza kulia akanambia  et nyumbani  mama anaumwa sana kwahiyo natakiwa kwenda nilikuwa sitaki kuondoka kukuacha wakati ndio kwanza umetoka safari 

Nilimwambia  mbona hakuna shida  mke wangu hakuna shida kabisaaa nenda nyumbani ,tutaondoka wote kesho asubuhi  akanambia  hapana we baki mie nitaenda kesho na kesho kutwa nitarudi akiwa vibaya nitakwambia uje

Tulielewana hivyo lakini kaka yake aliondoka bila hata kuaga na wala hakunisemesha alikuwa kama ana hasira  sanaaa  
Nikamuuliza dada yake vipi  akanambia achana nae basi mie nikaachana nae

Asubuhi nilimpeleka mke wangu  standi ili aende kwao yeye kwao ilikuwa ni mtwara  .


  Siku  zote nilikuwa naamini wanawake wenye elimu ni wasumbufu wanawake wenye kazi siwawezi mke wangu nilimpata tu mtaani mwanamke wa kawaida sana na nilimpenda sanaa ..

  Shemeji yangu alikuwa anakuja kazini lakini  haongei na mimi kama mtu mwenye  hasira

Na zilikuwa sikumbili tangu dada yake aondoke  nyumbani  kwangu

   Nilipo toka kazini ile usiku niliamua kwenda nyumbani  kwa shemu ili niongee nae mana nilihisi ana tatizo  na mimi kabisaaa

  Nilifika mpaka nyumbani  kwake mhu ajabu sana sana ile siku naiona kama jana tu

Share kwa ndugu na marafiki

WhatsApp
Facebook
Twitter

Chagua kipande kinachofuata