CONNECTION YA BALTASAR (05)

SEHEMU YA 05
  
Akanambia  nikuache basi ulale  nikasema sawa mana nasinzia hapa hatari ndio akakata simu mie usingizi ukanipitia

Nimekuja kushtuka asubuhi  nakuta text et ulale salamaa mmmh huyuu nikatabasam tu bwana  , nataka kuifuta kuna text ikaingia M pesa  nimepokea 15000 kutoka kwa mussa mmh😞😞 jamani wakati bado nashangaa ikaingia text nunua Vocha bint et uwe na asubuhi  njema

Hee hadi kujibu nikashindwa nijibu  niniii??
  Unajua Elfu kumi na tano kwangu ni kama  milioni eeh nishazoea jero jero naa jero  yaan mia tano ya Tanzania mie kuishika kwangu ni mtihani sana sasa hela kama hizi nawehuka

Nilimtumia sms Asante  sanaaa lakini naomba usinitumie tena pesa mama yangu akijua anaweza hata nichunja hapendi mno , na simu yangu anaishika mara kwa maraa

Akanijibu muda huo huo akanambia  mmh jamani I wish nimuone mama nimpe Hongera amekulea vyema mpaka raha umekuwa kama sio bint wa Dar

Mie nikacheka kwa emoji tu sikuandika kitu akanambia sijakuuliza hata jina mhu unaitwa nani cxx
Nikamwambia  naitwa Dixfxnxxxa mie akasema  Hata kajina kazuri sauti nzuri hivi huyu bint atakuwaje  si atakuwa zaidi hata wa yule malkia wa uingeleza🤣🤣🤣🤣🤣

Ila wanaume jamani 🙌🙌🙌🙌🙌 hapanaaa Nilichekaaa sanaaa nikamwambia  walaa mie wakawaida tu akasema Wish nikuone siku moja nikamwambia inshaallah  tutaonana bwana Mussa

Akacheka kwa Emoji akanambia D mamaa nitakuchek mida nipo kibaruani hivyo nisije fukuzwa kazi bureee 
  Nikasema sawa kazi njema akasema sawa mamaa et akaweka na emoj ya kuchumu😘

Makubwa 🙌🙌🙌  sijawahi mie kuchat na Boy yeyote zaidi ya mashost kwahiyo haka ka moments  nilijiona kama kiasi flani nimebadilika yaan nimependa😜😜 

Mana muda wote nilikuwa nazipitia pitia Ile text😂😂 mtu mwenyewe hata simjui lakini basi tuuu anafurahisha

Mchana akanitex hello

mmh nikajibu fast hbr
Akajibu poa babyy umekula??

🙄🙄🙄Babyyy tenaaaa??? )Nikamuuliza kwa mshtuko akanambia 

Baby I mean mtoto jamani we si unakisauti kama mtoto jamani hata hivyo hujatimiza miaka 18 so we ni Babyyy😀😀😀
. Ila huyu kaka 😂😂😂 nikaona aibu nikajichekesha kwa emoj  kama zotee 

Akambia Umeshakula babyy

😀😀😀nikajibu bado

Akanambia kwanini nikamwambia  ni mapema sana sa hii sa sita hii jamani akanambia  kwani chakula cha mchana wanakula sa ngapi?? Nikasema sa nane au Tisa 

Akasema🙄🙄weee hicho mbona cha usiku nikamwambia  basi tumetofautiana mie cha usiku sa nne kabisa  akasema hee wewe unalala sa ngap nikamwambia  muda wowote  tu akanambia  nakutumia hela basi ule hata viazi hapo mie sijiskii vizuri nakula wakati baby yupo njaa

😀😀😀Nikamwambia  mie sisikii njaa bwana chai nimekunywa muda huu akasema  hee basi mie nakutumia unywe hata soda😀😀

Nikawaza  huyu mbona ameng’ang’ania sana kunitumia helaa?? Ujue ndio wanatolewa kafara watu hivi hivii hakiamungu  nikamwambia  mie hapana usinitumie mama yangu atajua na anaweza hata nitoa kichwa akacheka kwelii kwa Emoji  akanambia  nakutumia  ndogoooo hata hawezi kujua ya soda tu please 

Jamaniiii 🙄🙄nikabaki nina mtafakari huyu vipii hata bado sijamjibu ikaingia sms ya M pesa imethibishwa umepokea Elfu tano kutoka kwa Mussa Mmh🙄🙄 nimepatikana mie aisee 

  Akanambia  nunua soda basi baby,mie narudi kibaruani kwani baadae bwana et

Hata sikumjibu aisee mie mbona naanza kuogopa  jamani yaan naogopa kabisaa

Yaan ile kuongea  kwangu  kila habari  ninayo lakini habari yangu nilikosa mtu wa kumsimulia kabisaaa
 
Niliona ngoja tu nimwambia mama lisije kuwa jini mie nikafa bure bila mama kujua lakini roho ingine inanambia nitaanzia wapi mie kumwambia mama yanguu??  

Nikatoka  chumbani kwangu  ilikuwa usiku  mama yupo ndani kwake , nikaenda kumwambia mama nashida ua kuongea na wewe akanambia  enhee kwemaa nikasema hata sio kwema mama kuna huyo mkaka sijui mba…..”

“Amekubakaa??” Mama aliniwahiii hata sijamaliza

Yaan mama yangu bora mniue maiti mpelekeeeni lakini sio kunibandua aisee hilo ni kosa la jinai kabisaaa

“Mama bwana ndo mana mie sipendi kukuambia mambo yangu we hata husikilizi”

“Embu ongea sasa haraka haraka unajibana bana ninii??”

  Nikamwambia  mama kuna mtu mie nilikutana nae Fb tu akaniomba namba yangu nikampa  si mjui wala hanijui ajabu ananitumia ma hela kila saa mie naogopa asije kuwa jambazii

Mama akasema  ma helaa??  Yaan alikutumia kama milioni ngap?? Ni mzungu au ??

Milioni tena🙄🙄🙄 nikamwambia mama sio milioni embu angalia ile siku alinitumia elfu kumi……

ITAENDELEA……

Share kwa ndugu na marafiki

WhatsApp
Facebook
Twitter

Chagua kipande kinachofuata