
SEHEMU YA 06
Milioni tena🙄🙄🙄 nikamwambia mama sio milioni embu angalia ile siku alinitumia elfu kumi leo asubuhi kanitumia elfu kumi na tano na mchana akanitumia elfu tano et ya Soda mi naogopa “
“Mxeewww ndio mahela hayoo, embu leta hapa hiyo siku kibaka tu huyo ameona Umeshakuwa mzuri uschana umekunawiri anajifanya kukutumia vijihela na wewe mpuuzi hivi ni vijihelaa sio ma hela utakuja kufa kwa vi chenchi chenchi tu “
“Ndo unanichamba😔😔”
 “Embu mpigie unipe anakujua sana huyu mtu mwenyewe anaonekana anamaisha magumuuu kama hakujui hawezi kujitumisha hela hovyo anakujua vizuri sana anachotaka hi huo Uc*** wako tu,Sasa wewe jichanganyee”
Yaan mama yangu unaweza hata kujuta kumwambia nimemwambia vizuri tu anaanza kunichamba mimi tena
Akanambia nimpigie na mie sikuw hata na salio bahati mbaya sana kwake nakwambia akapiga simu bila kujua tupo kwenye kikao na mama yangu
Mama akaiwahi ile simu
“We mpuuzi wa kiume wewe usie na haya na ma bint wa watu mbwa wa kinyamwezi wewe mpumbavu wa kiume tena wewe kaka wewe sitaki kwa bint yangu sitaki nasema sitaki kwa bint yangu hivi unanielewa???……….”
Â
😂😂😂😂😂mama aliongea mfululizo utasema amemeza Flash halafu sasa aliweka sauti kubwaÂ
“Haloo halooo haloo!!!” Mama akaanza kuita baada ya kuona kimyaa yaan hapo kashongea mpaka mate yamemkauka kabisaaa lakini mtu kimyaa
“Ahhmmm Samahani mama yangu Samahani sanaa , nimevuka mstari wa heshima sikupaswa kumtafuta hivi naomba sana unisamehe mama yangu”
Yaan aliongea kistaarabu mpaka mama mwenyewe aliona aibuu🤗🤗🤗Akabaki kujiuma uma tu et enhee wewe naniii akamwambia mie naitwa mussa mama , anhaa musa wa wapi et 😂😂😂yaan mamaaaa🤣🤣🤣 alivyobadili upepo gaflaa
 Akamjibu aah mama mie naishi huku mbezi aah baba sawa basi usiwe unafanya hivyo mie sipendi mwanangu kudanganywa danganywa Â
Yule kaka akamjibu sawa mama nimekuelewa naomba sana unisamehe !!
 Mama yangu akawa mpoleee akakat simu nikamwambia enhee mama yale ma tambo yako vipii?? Akasema embu koma wewee😂😂😂 Nikasema hayaa nimekoma akanambia embu nipe hiyo simu akai block ile namba halafu akaifuta kabisa akanambia akikutafuta tena nambie mpuuzi huyuu et mamaa! Nimemzaa mimi🤣🤣 nikamwambia mama mbona umeshindw kumchamba yeye jamani mie niache bwanaaa akanambia ila Dina bado mzima eeh nikamwambia mama mie mzima bwana hata sijafumuliwa
Nikaondoka zangu kwenda ndani vile mama alikuwa ameblock ile namba hakuna shida wala hakunitafuta tena
Asubuhi mama ananiambia et ile hela niirudishe kwa mwenyewe yaan mamaaa akhaa nikakataa mwenzangu ninatoa nikamwambia ww mimi naitumia akasema utakoma kama ni muhuni vitakutokea puani ,,, ahyaa haina shida huyu kaka hata sio muhuni
 Basi mie nikasahau tena habar za yule kaka kabisa nikaendelea na maisha yangu
   Sa siku moja  nilitoka kulikuwa na harusi jirani tulienda kuoa mbali kidogo na nyumba mie nilikuwa upande wa baba harusi anakaa mtaani kwetu huko
Nikiwa huko kuna namba ngeni ikapiga nikapokea bila hata kufikilia mara mbili
 “Samahani Dinaa naomba kuongea na wewe ” nilimsikia kwa shida sauti ya kiume lakini sikumjua na vile kulikuwa na makelele mie nikasogea pembeni nikamwambia we nani akanambia mussa hee moyo ukafanya paaa🙄🙄🙄Â
Nikajifanya kuuliza mussa ganiii???
 Akanambia yule uliemchoma kwa bi mkubwa wako😔😔😔nikaona aibu nikajufanya anhaaaa kumbe weweee enhee nambie
Akanambia naomba kuonana na wewe kama hutajali🙄🙄🙄 aliongea Serious wala hakuwa anacheka cheka tenaÂ
Nikasema kwani we upo wapi akanambia nambie wewe muda wako mie nifakufata hata ukinambia sasa hivi
Nikamwambia nipo harusini mie akanambia wapi nikamwambia nilipo akaniuliza mama yupo nikamwambia hapana akasema natokea hapo sawa nikasema sawa
Yaan hapo nishatepeta hamu tena sina kukataa naogopaa najionea aibu tu mie
All Rights Reserved © | Simulizi TAMU