CONNECTION YA BALTASAR (09)

SEHEMU YA 09

Mama akaniuliza we Mbona unanukia sana, Si nikakumbuka ule muda mussa alikuwa ananishika shika

Ndio akanikumbusha niliondoka mbio bila hata kumuaga hivyo 😔😔😔 nikamwambia  mama Si yule Vidia amekuja na pafyum yake ndio nikajipulizia mama akasema embu muulize  inauzwa shingap nzuri kweli na sie tuwe tunanukia mwanangu,Muulize jina nitamuagiza Muha 😅😅😅 nikamwambia  mama sawaaa nikimuona kesho nitamuulizaaa

Nikaingia ndani fasta nikamtext mussa
Umeondoka??🤗🤗 akanambia  umeniacha Njia panda naelekea wapiii nipo naangalia tu njia labda utatokea hapa au kulee
  
Nikamwambia  we nenda mie nishaingia kulala,,akasema Oooh umelala hata sijakukisi jamani vibaya hivyo
    
   Nikamwambia nenda siku ingine akanambia unaniahidi eeh nikacheka nikakata simu😀 nikaikumbatia simu🥰🥰🥰🥰
   Yaan nasikia et Rahaaaa😅😅😅walai sijawahi kuwa mpuuzi kiasi hichi

Ikaingia text Nimefika Dina nimefurahi sana kukuona asante
Nikamwambia  shukrani pia
Akanambia  Dinaa ujue mie nakupenda sanaaaa yaan siwezi kuendelea kukuficha

🙄🙄🙄 mwili ukaanza kutetemekaa sasa najibu nini akatext Haloo
  Nilikuwa kimyaa hata kujibu tena nashindwa niandike nini

Kweli mie nimetongozwa sanaa yaan sanaa kwa siku naweza tongozwa na vijana  kibao na kesho wakarudia bila kuchoka lakini sijawahi hata kufikiria  wala kuwahisi ni wanaume

Lakini huyu mwanaume huyuuu Halooo siwezi  hata kuelezea The way navyo Feel kwa huyu mukaka mpya  nina Vibee hatari  kuna kama mdudu ananitekenya tekenya mwilini mpaka ndani ya moyo🥰🥰🥰🥰🥰🥰🥰

Akanambia  naomba nikupigie , kabla sijajibu simu ikaita yeye ndie alikuwa  anapiga nikajitupa kwanza kitandani  nikagala gala nacheka  mwenyewe  baada ya kutengeneza koo ndio nikapokea
 
Hapo nipo chini  ya shuka n
Ndio nikapokea simu naongelea Tumboni yaani kisauti achaaaa🤗🤗🤗🤗

  “Haloo!”

“Dinaa”

“Abee”

“Nimekumiss mama yangu”

Uwiiii😂😂😂😂😂😂Nilisikia mwili kama umepigwa na shoti nikajibu “asante” yaan hiyo sauti kwanzaaaa unaweza sema nina vimafua kwa mbaliiii🥰🥰🥰🥰

“Kwani we hujanimiss??”

“Nimekuona sasa hivi tu”

“Mmmh kwelii mie basi nimeona kama vile tumeonana mwaka jana et”

😂😂😂ila wanaumeeee🙌🙌🙌Vichwa vyenuuuu 

  Kabla sijamjubu simu ikakata hata sijui kwanini😅😅😅 Roho ikaniuma nikusubiri  nipigiwe wapii subiri na kusubiri wapiii🙌🙌

 

Nina hamu ya kuongea nae hatari mpaka roho inaniuma wee nikasema hapana nikaenda  kwa mama hapo ilikuwa usiku umeenda  lakini sikuweza kuvumilia hata  nikamwambia  mama embu naomba simu yako akasema ya nini   huku anafoka hata sikumjibu niliichukua nikakimbia nikaenda kujifungia chumbani kwangu

Akabaki ananichamba mie hata sisikii nikaweka ile namba ya mussa kuipiga nikabaki najishauri sasa namwambia ninii??🤔🤔

Akipokea nitasema ninii?? Si ndio nitaonekana mie rahisi,  Mana hata kutongozwa sijatongozwa hivyoo😥😥Lakini mie nampenda huyu sijui mbaba sijui mkaka atajua yeye mie nampenda kichwa kuuma na vile alinambia ananipenda ndio basi tenaaaa🙌🙌🤗🤗😫🤗

Nikajikaza baada ya kujifikiria zaidi ya nusu saa nikapata pa kumuanzia nikapiga ikaita kidogo  ikapokelewa haloo sauti nzito nzito moyo ukafanya paa mussa wangu huyoo kapokea🥰🥰🥰🥰🥰🥰🥰🥰🥰🥰🥰🥰

Share kwa ndugu na marafiki

WhatsApp
Facebook
Twitter

Chagua kipande kinachofuata