CONNECTION YA BALTASAR (13)

SEHEMU YA 13

 Nikasema na hao ndio wanaume wenye maisha yao bora hata nngempa moyo  hawa wahuni wa mtaani kwetu huenda ninge enjoy zanguuu

Basi mpaka panakucha hivii mie macho kodo sikulala kabisaa , mama akanigongea niende kunywa chai sina hamu hata ya chai nikamwambia tu mama nakuja akasema sawa 

  Nilipo toka nikam_mendea ameenda kuoga ile nikachukua simu yake , nikaweka namba ya mussa mana tayari  nilikuwa nayo kichwani  hapo wazo lilikuwa ni kumbembeleza tu nitafanyaje sasa nimeshindwa kabisa kumsahau

  Nilipiga sana namba ya mussa haikuwa inapatikana 
  “Et nipo tayari  kufukuzwa kazi kwa ajili yako”😫😫😫mfyuu niliyakumbuka haya maneno ila nyie wanaumee🙌🙌🙌 

Nilipiga na namba yangu haikuwa inapatikana pia , ilikuwa ndio kazi yangu sasa kila siku kuipiga namba ya mussa na haikuwahi kupatikana mpaka nikawa najiuliza  kwahiyo alisajili na laini ili tu anipate mie daah

   Yaani ndani ya wiki moja tuu nilikuwa tayari nimekonda Uso hauna nuru kabisa mie mtu wa mawazo sanaa sanaa , mama aliniweka vikao na vikao alinisema mpaka basiii

Lakini sio mie ni moyo yaan moyo umeshindwa kabisa kuliacha hili swala kabisaaa , Wiki ya pili ndio hali ikazidi kuwa mbaya mpaka mama akaanza kuogopaaa sasa akawa anaongea analiaa
Mie nishakuwa mtu wa kujitenga tenaa mama akanambia  unapakumbuka kwa huyo mtu nikasema ndio mama aka akanambia  kesho twende huwezi kuteseka hivi bora akaniuwe nikasema sawaa mama

  Asubuhi ile ndio ilikuwa siku ya kwenda niliamka naumwa sana yaan natapika tu natapika sanaa
  Mama akanichukua safari ya kule ikafa tukaenda hospital  mana mwili ulikuwa hauna nguvu kabisaa

   Hospital  ndio  nilizidi kudata nyieee🙌🙌🙌Et mimi nina mimba uwiii😫😫😫 Nikajikuta  namwambia mama nimeisha mie nimeishaaaaaa mama yanguuu

Nilihisi kuchanganyikiwa  😫😫😫🙌🙌 mama akanifokeaaa akanambia embu tulia unafikiri  kuchanganyikiwa ndio kutatua tatizo au kulia ndio kutatua embu nyamazaaaa

Alifokaa mpaka watu wakageuka kututazama akanambia , huyo mtoto ni wako unataka kumuona ni mkosi??
Mungu ndio anajua kwanini amekupitisha hapo usijione unamkosi ilikuwa lazima upitee hapo

😔😔😔Daah yaan mama yangu alinilinda siku zote  hichi ndio alikuwa hataki  mimi nizae nyumbani  lakini nimemuangusha vibaya sana

Hatukwenda nyumbani  baada ya kutoka hospital  tulienda kwa ma mkubwa ,  mama akamwadithia ma mkubwa kila kitu ma mkubwa alishauri kuwa mama anipeleke kwa mwenye mimba na akikataa twende police  mana mie bado mdogo  sina miaka 18
   
Mama akasema kesho asubuhi  tutakwenda huko ilikuwa leo twende ma mkubwa akasema tutaenda wote mama akakataa akasema hata tusikusumbue wacha niende tu mimi …

  Tulishinda kwa mama mkubwa hiyo siku mpaka usiku kabisa tukala na chakula cha usiku ndio tukaondika kurudi mida ya sa nne hivi usiku ..

Tumefika nyumbani  jirani wa chumba cha nyuma akamwambia mama kuna mtu alikuja hapa kuwatafuta  mlivyotoka tu na ameshinda hapa kuwasubiri ametoka muda sio mrefu yaani mmepishana hapaa
  
Mama akauliza ni nani yule dada akasema mie hata simjui ndio kwanza nimemuona ni mwanaume mkaka hivi
Mie moyo ukafanya paa sio mussa kweli nikawahi kumuuliza yupoje

Akanieleza huyo mtu alivyo , hakuwa hata anaendana na mussa wangu 😭😭,nikahisi  maumivu kuanza upya tenaa

   Alikuwa ameacha namba yake ya simu  mama akaipiga iliita ya kwanza ikakata ikaita ya pili akapokea mdada akasema  mwenyewe ametoka kidogo  akija atampigia  mama akakata bila hata kuongea akanambia  nenda kalale …

   Asubuhi  kabla hata jua kutoka mama alikuja kuniamsha akanambia  jiandae tunaenda 
.  Nilipata nguvu nimemkumbuka mussa nina hamu ya kumuonaaa🤗🤗🤗Nimemiss na kuwa na mimba yake nilikuwa na furaha mnoo  sikujali atakataa au kukubali wacha niwe hata na mtoto wake tu inatosha 

  Tulienda mpaka hapo nikaikumbuka nyumba vizuri tu , yaan nilivyoona geti lilee miguu ikaanza kutetemekaa woga wa kukataliwa tena nikaanza kuuhisi upyaa
    Nikakumbuka jinsi mussa alivyoniingiza kwa mahaba ya kubebwa juu juu  na nikatoka kwa kilio hii nyumba siji kuisahau miee

  Mama akanambia  unauhakika ndio hapaa?? Nikasema ndio hapaa akagonga geti mara ya kwanza mara ya pili likafunguliwa
   Uso kwa uso na Sulee alipo niona alishtukaa🤔🤔🤔
  Akababaika mama akaniuliza ndio huyuuu?? Nikasema hapana mama akamwambia  hayaa wewe huyo mzee wa kujaza watoto wa watu yupo wapiii ,mama akanigeukia akaniuliza anaitwa nanii?? Nikasema mussa huku nimeinamisha uso wangu chini

Mama akamgeukia Sule akamwambua hayaa umelisikia jina lake yupo wapii.?

Sule akasema mama naomba tuingie ndani tafadhali 🙏🙏🙏 mama akamwambia  yupo hayupoo??
Sule akasema hayupo lakini tunaweza kuongea mie ni mdogo wake mama akamuuliza  huyu unamjua wewe??
  Huku ananinyooshea kidole

Sule akasema ndio ni Dina ninamjua vyema sana japo tulionana mara mojaa tu ..
    Mama akasema  haya tunakwenda tutarudi mwambie huyo mpuuzi  nipo nayeye mpaka mwisho

Sule akasema hapana mama usiondoke naomba sana tuongee
Mama akamwambia mie sina cha kuongea  na wewe namtaka aliemtia mwanangu😀😀😀yaan mama et nimetiwa 😂😂😂 
 
  Sule akasema mama naomba tuongee jana nilikuja mpaka nyumbani  kwetu nilihangaika sana kupapata lakini sikuwakuta nilisubiri siku nzima hamkuja nikaacha namba yangu ya simu bado sikupata simu zenu

  🙄🙄🙄🙄🙄🙄Kumbe huyu ndie alikuja nyumbani?? Sasa alikuja kufanya ninii??
Nikajikuta nina maswali kibao huku naombea mama akubali tumsikilize kwanini alikuja nyumbani jana

Share kwa ndugu na marafiki

WhatsApp
Facebook
Twitter

Chagua kipande kinachofuata