CONNECTION YA BALTASAR (15)

SEHEMU YA 15
 
 Shemu akanipanga sana akanipa mbinu za kuhakikisha bro wake namshika  haswa

Sule akanambia  mussa ndoto yake ilikuwa siku moja kuwa baba anatamani kuwa na mtoto ninafuraha kwa ajili yake mie wala sintamwambia kama wewe ni mjamzito  nataka alisikie kutoka kwenye kinywa chako🥰🥰🥰🥰🥰

    Akanambia  shemu mtooto hakusumbui😂😂😂 jamani 🙌🙌 nikasema natapika tu
Akanambia  basi jioni nitakuletea kitu kitamu ule huyo itakuwa amemiss bab yake🙌😂😂😂nikawa nachekaa huyu mtu na ndugu yake wote  wanavituko akanambia jioni nakuja mke wetu nije nimuone mtoto wetu

Nikamuuliza  et shemu kwani mke wake na musa alifanya nini, sule akanambia mmh embu atakwambia yeye akihitaji kukuambia lakini mie nisivuke mipaka

  Jioni shemu alikuja 🥰🥰🥰Akaniita sehemu hakufika nyumbani alisema anamuogopa mama akaniletea ma pocho pocho nilikula hatari nikarudi nyumbani  mzitoo

Nafika nyumbani si ndio namkuta kaka🙄🙄nikasema moyoni huyu  nae usiku usiku anakuja nyumbani  kwanza hata sijui kaja lini dar 🤔🤔 nikamwamkia shikamoo  kaka akanambia  embu kaa hapo yaan hata bila kuitikia salamu yangu

Nikasema moyoni kumekuchaaaa
Kaka akanambia  we dina umeshindwa kabisaaa kujituliza yaan umeshindwa mpaka unatuletea mimba hapa nyumbani??  Mimba za utotoni??

“Kaka naomba  unisamehee,Ni bahati mbayaa”

“Kwahiyo ulijikwaa ukadodokea mimba eeeh??……..wewe si nakuuliza …..naongea na wewe dinaa!!! …..kimya ndio kinamaanisha niniii??”

Kaka sijui alitaka jibu gani kutoka kwangu , anajua nilifanya nini nikapata mimba  afu ananiuliza et nilidondokea😅😅😅kwahiyo nimjibu niliikalia auu?? 🤣🤣

Mie  nilikuwa kimyaa nimejiinamia chini majibu sina
Akasimama akafungua  mkanda wee nilipiga magoti fasta nikaanza kulia
Mama akamwambia Jose naomba  usimpige huyo mtoto tena nitolee ujinga wako
Kaka akamwambia  kwahiyo ulikuwa unaniambia ili iweje kama ulikuwa  hutaki huyu mtoto akanywe angekuwa mtoto angeenda kujibinua huko abebe hiyo mimbaa
  Mama akainuka akaja kusimama mbele yangu akamwambia hakuna maana kama kosa limeshafanyika hapa tuangalie jinsi ya kumtunza huyo mtoto basi kupiga na mtu yupo kwenye hali hiyo unataka kuniletea mie matatizo eeeh”

“Mama kaa pembeni sioni kazi huu  mkanda kukufikia weweee”

“Kwahiyo unataka kunipiga si ndio”

“We Dina toka hapoo??”

Yaan et nitoke nyuma ya mama aah weee ndio kwanza nikajitengeneza vizuri  kujificha🤣🤣🤣wenyewe wapigane tu si mtu na mama yake mie nifanyaje

  Kaka akaanza kumsukuma mama ili anifikie mie wee na mie mama atakapo sukumwa ndio nafata huko huko kaka ananiambia  dina nitakufumua nitakufumua weweee njoo hapa nikasema hata siji kaka 

“Unasemaje wewee??”

Nikakimbia chumbani kwangu  nikaenda kulala kaka akabaki anasema kwa jazba  kweli yaan roho ilimuuma kwanini hajanifunza adabu🤣🤣embu anipishe mie asubiri watoto wake awafunze kwa kujinafasi

Nikalala zangu ndani kimyaa nikaacha mama na mtoto wanagombana mama akajuta kwa nini alimshirikisha kaka

Basi kaka akanambia haondoki hapo nyumbani  na mie nijifungie ndanu maisha yangu yotee🤣nikamjibu sawa ngoja nifie humu ndani

Mama wacha aanze kulia et Dinaa usijiue mwanangu😅😅yaan mimi huyu nijiue mimiiiii?? Hee aah wapiii

Mama akabaki anamlaumu kaka nikifa atanila nyama analia mlangoni kwangu anagongaa mie kimyaa

Yaan hiyo siku tukawa kituko kwa majirani na bahati nzuri sie ndie mwenye nyumba ingekuwa tumepanga sijui ingekuwaje tuu

Share kwa ndugu na marafiki

WhatsApp
Facebook
Twitter

Chagua kipande kinachofuata