CONNECTION YA BALTASAR (16)

SEHEMU YA 16

 Mama alinigongea hata niende kula hakujua kama nishakula huko niko ndii nikamwambia hata chakula chenu siliii🤔🤔😔

Basi kaka ndio anazidi kubebeshwa lawamaaa😅😅yaan mama na alimuita yeye mwenyewe  hapo ..

   Nikalala zangu mie hata sikujua wamemaliza vipii

Asubuhi  sikutoka nje mama ananiita njoo unywe chai nasema sitaki  kaka atanipiga mama ananiambia  we Dina embu njoo hawezi kukupiga mie nipo hai hawezi njoo  namie nimekaza sijiii alinambia nifie humuu😔😔 ngoja nife mlizike 😅😅😅

Mama anasema  jana umelala njaa Dina na hiyo hali yako embu njoo we Dina wewe
Mie kimyaaaa

Mara nikasikia li sauti la kaka

“We mpumbavu wewe haraka toka humo ndani hakuna wa kukubembeleza, nikivunja hichi kitasa dina mama yako hatoweza kunizuia hivi unanielewa”

Mmmh 😅😅😅alivyoongea sauti ya kiume aaah weeee nikajua hapa navunjwa mguu wallah 😂nikafungua mlango mwenyewe 

Kaka akanisonya tu wala hakuongeza neno , mie nikachukua chai nikanywa zangu kaka baada ya chai akaondoka zake et akamwambia mama kila akiniona anasikia  hasira hawezi  kukaa na mie karibu😟😟😟😟

Mama akamwambia we nenda tu mie nitamaliza na mwanangu  mwenyewe  kaka akaondoka analalamika et mama ananiendekeza  ..

  Kaka alipoondoka mama akanambia  haya we nae njoo unifatie vocha  hapaa nikatoka kufata vocha

   Wakati natoka dukani nikasikia naitwa

“Babyyy Dinaa” kamoyo puu💗 nikageuka fasta sikuamini namuona  baby daddy wangu mtarajiwa 🥰🥰

Tena ananitazama kwa tabasam kama sio yule alienipa stress  wiki mbili zotee

Nilikimbia  mwenzangu nae akatanua mikono  yake  nikajichomeka chap akani hug🤗🤗🤗
  Akanibusu mpaka basi

“Dinaa mamaaa et una mtoto wangu ???”

🙄🙄🙄Hee huyu shemu si alinambia hata mwambia nimwambie mwenyewe  imekuwajeee??

“Umejuajee”

“Dinaaaa embu njoo kwanzaaa”🥰🥰🥰akanibeba juu juu yaan hapo ni asubuhi  mtaani watu  kibaooo halafu mussa  analeta mahaba ya kitajiri yale ya kwenye Tv😅😅😅😅

“Sitaki wewe si ulisha nikataa”😔😔😔😔 nikajitoa hapo tayar nishanunaaa ila sio Serious

Zuchu alisema hivi  kuna wimbo wake flani hivi (nikinuna mie ndio nadeka usije dhani kiburi ukanacha nije kuchekwa) 😂😂😂

Sasa mie ndio nilinuna ule mnuno wa kudeka😅😅😅
Akanivuta nikaangukia kifuani kwake 
“Mama mtoto wangu naweza kukuelezea tafadhali “

“Sitaki hata maelezo yako”

“Noo!!!Dinaa” si akanipiga busu la mdomo🤗🤗
Sasa mie ndio akili ikaja nikagundua kuwa robo tatu ya watu wote wanatutazama sisi nageuza macho ili kutazama vizuri  mamaaa🤔🤔🤔 

Nakutana uso na macho na mama yangu salaleee ameshika kiuno anatazama jicho kalioi🤦‍♀️🤦‍♀️🤦‍♀️

Nikajitoa fasta kwa mussa “mamaaa!!!?”
Mussa kusikia mama aloo😅😅😅aliruka nyumba kama hatua 7 za gafla mnooo

  “Nimekuja kuongea na mama naomba unipeleke nyumbani ” akabadilisha na sauti kawa mwema sana  

“Twende” na mie nikajibu kama wa maana vileee

Mama hakuongea kitu akarudi zake nyumbani  basi tulikuwa tunatembea kimyaa kama tumejisaidia kwenye nguo kila mtu ana haya kivyake

Nikamfikisha nyumbani  mama alikuwa amenunaaaaa kama anamjua mussa vile kumbe hata hajawahi kumuona 

“Hiyo mimba haitoshi umeanza na kunitia aibu mtaani kufanya mapenzi hadharani sio”

“Mamaaaa!!!”

“Mpumbavu weweee mbona unanudharirisha sana Dina”
  Daah😔😔😔😔 Ilibdi tu nikae kimya tusibishane mbele ya mgeni

Nikamwambia mussa karibu huku nampa kiti mama hata hakumkaribisha alikuwa anamtazama kama amejisaidia mbele yake bila kutoa nguo

  “Mama huyu ndio mussa yule tulienda kwake  juzi” 
  Mama alimtazamaa yaan kuanzia chini mpaka juu kwa sauti ya  kuchoka akamwambia

“Karibu,  haya kimekuleta nini hapa??”

Hee mamaaa😔😔 Nilijisikia vibaya  kweli hata hamkaribishi vizuri  angejua mimi huyu kaka bila yeye siwezi kuishi basi tu
Angemtetemekea kwa ajili ya uhai wangu

Share kwa ndugu na marafiki

WhatsApp
Facebook
Twitter

Chagua kipande kinachofuata