
JOGGING MASTER (05)

JOGGING MASTER ππ5
(Master of loveπ)
ππππππππ
Yule mkaka bwana alikuwa kavaa zake bukta na singlend alaf mkononi alishika chupa ya maji……
Tulikuwa na njaa Kali sana hatukumzingatia kiviiile sisi tunawaza kula tu π€£π€£π€£
Tulitembea hao tukatokezea sehemu za madukani na biashara mbalimbali….Tulianza kutembelea migahawa mmoja baada ya mwingine ilimradi tu tusikose kitu. …..
Tulipata sehem moja ya mgahawa palikuwa na Wateja wengi sana tukaambiwa mmoja ataosha vyombo na mwingine amenye viazi vya chips debe sita alafu jion malipo ni elfu mbili kwa kila mmoja π€£π€£ ,
“Lakin dada tunaomba hata chai kwanza Jana usiku tumelala na njaa ,nilisema kwa maana sikuzoea kulala na njaa Mimi ππ
“Sawa mtakunywa chai na kiporo Cha ubwabwa lakin hakina mboga alisema na kutuonesha sehem ya kwenda kupata chai …tulienda tukapiga chai na ubwabwa na maharage haoooo kazini sasa π….
“Haya chagua utafanya kipi ,maombi aliniuliza …..duh afadhali nioshe vyombo tu ila kumenya viazi debe sita ni nyingi mno ….maombi alinitizama na kusema
“Fanikiwa unayajua maisha ?? Usichague kazi as long as una uwezo wa kuifanya haijalishi ni ngumu kiasi Gani just do it mkono uende kinywani alisema na kusogea zilipo gunia za viazi,alichukua kisu na kuanza kazi….na mm nilisogea vilipo vyombo mana vilikuwa ni vingi balaa vya tangu Jana …tukaanza kazi vitoto vya mafukara π€£π€£π€£π
aisee Maombi ni hatari huyu dada alipiga kazi Yan viazi vinamenywa kama vipo kwenye machine ππ, Yuko faster balaaa …niliwah kumaliza vyombo na yeye alikuwa Bado anamenya niliomba kisu na kuanza Kusaidiana alooh huyu mwanamke ni wife material π …..anapiga kazi na akiwa kazini hataki kuongea ongea yeye Ni mikono tu ndo inayoongea ππ
Nilijifunza kitu kikubwa kwa yule Binti anaakili sana na nimchapa kazi wa viwango vya juu kabisaaaa
Basi mchana Wateja walifurika pale kwenye ule mgahawa na sisi tukiwa bize na kazi mpaka kufikia saa kumi na moja jion kila kitu kilikuwa tayar na chakula kilikuwa kimeisha ……
“Safi sana nyie nimewapenda Bure mnafanya kazi vzr sana hamna utani kazini alisema yule mdada ambae ndo boss wetu
Akatuuliza tunatokea wapi …..
Tulipomwambia sisi ni wanachuo alivunja mbavu π€£π€£π€£
“dah mbona mmeanza chuo kwa uchungu hivyo ? Yan maisha yamewapiga mapema yote hii ? kiasi Cha kuja mtaani kufatuta kazi πππ?
“Dada we acha tu tunasubr boom kama tutapata ,tukikosa basi tutaendeleza kibarua chetu hapa …nilimjibu
” Dah karibuni sana wadogo zangu mjiskie mko nyumbani sawa ,ingieni ndani mle chakula niliwatengea ndo muondoke alisema ….
“Sawa dada tunashkuru sana …tulipata chakula wali nyama ya kushibaaaaa ……. alitulipatia malipo yetu na tuliagana nae haooooo tukaondoka zetu kurudi chuo kulala ππ
Tulipita njia ileile na kwa mara ya pili Tena tulikutana na yuleyule mkaka Wa jogging π alikuwa kabadili nguo zake ….hatukumjali kama kawaida kila mtu na mambo yake mjini hapa πΆ …..
Tulifika chuoni tukaagiza soda tu maana tulikuwa vitumbo ndiii tumeshiba hao hatari , tulilala zetu fresh kabisa ……
Asbh na mapema kasimu ka Maombi kaliita na namba ilikuwa ni ya baba yangu ….
Nilipokea ……
“Mwanangu yule mteja wa mbuzi ameniangusha sana, nitafanya maarifa mengine lakini naomba nitakutumia elfu Tano baadae saa nne asubuhi angalau ikusogeze kidogo π’ alisema baba ….
“Sawa baba hakuna shida Mungu awasaidie mfanikiwe baba angu , nikamwambia
“Asante mama Mungu akulinde na kukuangazia Nuru yake usikate tamaa π’π’π’π’
Tuliagana na …..
bas mimi na maskini wangu tukajiandaa kwaajili ya kwenda zetu kazini hahah no time to west men π€ haooo wanawake nangai tukashika njia kwenda upande wa mashariki π€£π€£π€£
itaendelea dears

