LOML | Love Of My Life (187)

π‹πŽπŒπ‹ (𝑳𝒐𝒗𝒆 𝒐𝒇 π’Žπ’š π’π’Šπ’‡π’†) ❣️:187

Dawa hazikuwa zinamsaidia kabisa mtoto wangu, alizidi kuwa na hali mbaya sana. Hali yake ilikuwa mbaya mno, mno kwa mtoto wangu.

Ilinibidi nirudi hospitali, walimfanyia vipimo mtoto wangu, lakini hakuwa anaonekana ana tatizo. Mimi nilikuwa nalia hata namuuliza dokta β€œkwani dokta mtoto wangu ana shida gani?”

Dokta huyu alinitazama, na kuniuliza β€œmtoto anaitwa nani vile?”
Nilimtajia jina lake, alinitazama na kusema β€œhuyu si wakiume?”
Nilimwambia kwa upole nikilia β€œndiyo ni wa kiume.”

Aliniambia β€œhili jina mbona maana yake sio nzuri kwa mtoto wa kiume.”
Nikauliza kwa upole β€œmaana yake nini dokta?”
Huyu dokta aliniambia β€œni nani aliyempa jina hili?”

Nikainamisha tu kichwa, basi huyu dokta alinaimbia β€œhuko kwetu maana yake ni mwanamke asiyeambilika.”
Nikashtuka na kusema β€œmwanamke asiyeambilika, Mungu wangu!!”

Huyu dokta alinitazama na kusema β€œsikia unaweza kusema mtoto anaumwa kumbe unatakiwa kuomba, mimi sijui sana. Chukua namba hii ya huyu mtu atakusaidia sana. Atakusaidia kwenye maombi yupo vizuri.”

Nilikuwa nashangaa tu, alinitazama na akaniuliza β€œna vipi macho?”
Nikamwambia tu β€œnimepata dawa dokta.”

Nilimshukuru sana na kuondoka nikiwa na hasira. Nilifika nyumbani mwanangu analia mpaka nachanganyikiwa. Nilimpigia bibi yangu simu nikamuelezea kila kitu.

Share kwa ndugu na marafiki

WhatsApp
Facebook
Twitter

Chagua kipande kinachofuata