LOML | Love Of My Life (197)

π‹πŽπŒπ‹ (𝑳𝒐𝒗𝒆 𝒐𝒇 π’Žπ’š π’π’Šπ’‡π’†) ❣️:197
Nilivuta pumzi na kisha niliendelea β€œMama babuu, jitahidi sana kwenye hilo. Nataka amani zaidi kuliko chochote kile. Kabla Sijasahau huyu mwanamke mzuri mbele yako unayemuona anaitwa Pina.

Huyu ndiyo mpenzi wa maisha yangu na huyu sasa ndiyo Madam wako. Yupo huru hapa muda wowote na wakati yoyote akiwa hapa tafadhali fanya kila anachokuelekeza. Anaitwa Pina.”

Mama babuu alitabasamu na kusema β€œnashukuru sana kukufahamu madam.”

Pina alitabasamu, na kisha niliendelea β€œPina anaitwa mama Babuu, ni mama yangu hapa nyumbani. Mama mzuri sana tafadhali nategemea mtaishi kwa upendo.”

Pina alitabasamu na kuniambia β€œasante sana mpenzi, nimefurahi kukufahamu mama. Mimi naitwa Pina.”

Wakapeana Mikono na wakati huo Pina alikuwa anatabasamu tu. Na mama Babuu alinionesha kidole gumba cha safi sana akionekana kuwa na furaha sana. Nilitabasamu nikisema β€œmama Babuuu, unaweza kuendelea na mambo yako sasa.”

Mama Babuu akawa anaondoka, hakufika mbali nilisema β€œmama Babuuu, naomba msaidiane na mlinzi tafadhali. Kule chumbani kitu chochote cha Gabby naomba kitoke. Na hata hivyo vitu vyangu hamishia chumba kingine, na kile kitanda kiondoke kabisa nitaagiza kingine sitaki kiwepo hapa nyumbani.”

Mama babuu alinitazama na kuniuliza β€œina maana kitanda?”
Nikamuuliza β€œuna kihitaji?”

Aliinamisha kichwa chini, na kisha nikaendelea β€œkitanda ni sehemu nzuri sana. Kama una hitaji siwezi kukukatalia. Ila tayari hiko kitanda kina roho kimebeba kama unaweza jitenganisha na roho hizo kichukue haina shida.”

Mama Babuu alitabasamu na kufurahia sana. Halafu Mimi nilimuongoza Pina aliketi.

Share kwa ndugu na marafiki

WhatsApp
Facebook
Twitter

Chagua kipande kinachofuata