LOML | Love Of My Life (10)

π‹πŽπŒπ‹ (𝑳𝒐𝒗𝒆 𝒐𝒇 π’Žπ’š π’π’Šπ’‡π’†) ❣️:10
Tulielekea kula, tulipofika kula mke wangu sasa anapiga picha kila kitu, mara nipige picha. Mimi tena ndiyo mpiga picha, chakula kinapigwa picha mpaka nachukia na ni muda wa kula. Alipomaliza alitabasamu na kusema β€œtule sasa Hubby.”

Nilishusha pumzi tu, alichukua uma wangu na kunilisha. Kisha aliendelea kula huku akiwa anazungumzia ndoa yetu namna imeenda viral, watu wanazungumzia, marafiki zake na zawadi.

Mimi nilikuwa nakula, namuwaza yule binti niliyemuona kanisani. Kisha nilikuwa nashindwa kabisa kujizuia kutabasamu. Nilijikuta natabasamu tena tabasamu pana kabisa. Mke wangu alinitazama na kuniita kwa Jina langu β€œRicky!!”

Mimi nikaendelea tabasamu, akaniita tena β€œRicky!!”
Nilimtazama na kusema β€œNaam!!”
Aliniuliza kwa kunishangaa β€œunatabasamu!!.”
Nikatabasamu tena na kumuuliza β€œkwani vibaya kutabasamu na mke wangu?”

Na yeye alitabasamu na kusema β€œkumbe nakufanya utabasamu, napenda hiyo mume wangu.”
Nilimtazama tu nikitabasamu kumbe mimi uzuri wa msichana yule ndiyo unafanya natabasamu na wala sio yeye. Moyo wa mtu kichaka. Tukiwa na hali hiyo mara simu ya mke wangu iliita. Aliitazama na kunitazama, nikamuuliza β€œkuna nini tena?”

Alishusha pumzi na kusema β€œni mama, sijui anataka kusema nini?”
Nilimtazama nikisema β€œpokea, labda wanakusalimia tu.”
Ndipo mke wangu alipokea simu, alipopokea tu nikaona uso wa mke wangu unapoteza furaha, nikamuuliza β€œkuna nini?”
Mke wangu aliendelea kusikiliza simu huku akinitazama kwa hofu, na kisha alikata simu na kusema β€œ πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚sa itakuajeπŸ€¦β€β™€οΈπŸ€¦β€β™€οΈπŸ€¦β€β™€οΈ

Share kwa ndugu na marafiki

WhatsApp
Facebook
Twitter

Chagua kipande kinachofuata