LOML | Love Of My Life (25)

π‹πŽπŒπ‹ (𝑳𝒐𝒗𝒆 𝒐𝒇 π’Žπ’š π’π’Šπ’‡π’†) ❣️:25
Tukiwa kwenye hii hali hata kazini nilijiambia mpaka niweke sawa na mke wangu nitaanza tena kazi kwa hali hii sitaweza, siku hii asubuhi ilikuwa jumatano hivi. Nilichelewa kidogo kuamka, nilipoamka mke wangu hakuwepo kitandani.

Nilitoka na nikashangaa nakuta yule mama wa kazi ndiyo anafua nguo zangu mpaka boksa, na nguo za ndani za mke wangu. Nilishangaa, nikamuuliza β€œsamahani, mke wangu yupo wapi?”

Akaniambia kwa heshima β€œyupo nyuma ya nyumba.”
Nilizunguka, na kisha aliponiona alisema β€œmume wangu, kuna nini mbona hivyo?”
Nikamuuliza kwa upole β€œunajisikiaje?”
Alinitazama na kusema β€œnashukuru Mungu naendelea vizuri kabisa.”

Nikaendelea β€œmke wangu tunaweza ingia ndani tukazungumza?”
Akanitazama na kusema β€œmume wangu, mama babuu itakuwa anafanya usafi.”
Nilimtolea macho na kusema β€œwhaaat!!”

Akashangaa na kuniuliza β€œni nini lakini mume wangu?, mbona unanishtua?”
Nilitazama huku na kule na kusema β€œIna maana mke wangu huna kazi unaweza kufanya. Kufua, sawa muache afue ndiyo mpaka nguo zetu za ndani?, kusafisha chumba unacho lala na mumeo na hiyo ni ngumu, bado hata siku moja hujawahi kuandaa chakula kwaajili yangu au yetu. Ni nini sasa.”

Mke wangu akanitazama na kucheka, halafu akanikumbatia akideka na kusema β€œsasa mume wangu shida ipo wapi, mimi mwenzako mambo ya kazi kazi za nyumbani hata siwezi. Mama babuuu nipo naye zamani sana hana baya lolote. Sasa wewe unahangaikia nini, muhimu namlipa vizuri tu.”

Nilivuta pumzi na kumuuliza β€œmke wangu, unajua kupika au hujui?”
Alinitazama na kusema β€œuna kuza sasa, mimi na wewe hata nyumbani hatushindi akipika yeye ndiyo naacha kukupenda kwani jamani.”

Nilimtazama na kutikisa kichwa changu, nilijihurumia ina maana maisha yote mke wangu hatowahi nifanyia chochote kwa upendo zaidi ya kitandani. Nikamwambia β€œG mke wangu, nakupenda sana. Najua umeishi maisha ya kufanyiwa kila kitu. Kuna raha ya wewe kunifanyia baadhi ya vitu vidogo vidogo kama chumbani kwetu kile ni chumba chetu mimi na wewe, nguo za ndani eenh ni wewe unifulie na kama ukitingwa bora nifue mwenyewe kuliko yule mama. Natamani wewe mke wangu ndiyo ufanye kwaajili yangu.”

Gabriella alinitazama na kusema β€œ

Share kwa ndugu na marafiki

WhatsApp
Facebook
Twitter

Chagua kipande kinachofuata