LOML | Love Of My Life (34)

π‹πŽπŒπ‹ (𝑳𝒐𝒗𝒆 𝒐𝒇 π’Žπ’š π’π’Šπ’‡π’†) ❣️:34
Kitu pekee unatakiwa kufanya kijana wangu ni kuipambania ndoa yako, kuhakikisha kΔ±la kiti kinakuwa. Sio rahisi mwanangu tena wakati mwingine ni ngumu haswa. Lakini usikubali kushindwa wewe ni mwanaume na ndoa yako hata mwezi bado tafadhali. Simama imara.”

Nilimtazama baba na kujikuta namuuliza β€œumewahi kukaa siku ukajutia kumuoa mama yangu, au kuhisi humpendi kabisa?”

Baba alinitazama kwa muda, nikaona macho yake yakibadilika. Halafu baba yangu alitazama chini. Nikaona anainua mikono yake na kujifuta machozi. Halafu nikaita β€œbaba!!”

Baba aliinua uso wake akitabasamu japo naona hayupo na tabasamu La awali na kusema β€œkuna mtu kijana wangu huna La kufanya kabisa una acha tu maisha yafanye vile yanataka. Ndiyo maisha. Inatokea Mara nyingi lakini sio sababu ya kuacha ndoa yako. Wakati mwingine suluhu ni kutulia tu.”

Nilimshangaa baba yangu, wakati huo mlango ulikuwa unafunguliwa, alikuwa mama akitabasamu na kusema β€œbaba na mwana, mna kikao gani cha Siri namna hiyo?”
Tulijifanya kucheka tu, halafu mama aliniuliza β€œUpo sawa lakini?”

Nilitabasamu na kusema β€œkabisa mama, hata hivyo nataka niwahi nyumbani.”
Mama alitabasamu na kusema β€œkabisa maana binti yangu alipiga anaonekana na wasiwasi sana. KΔ±la kitu kipo sawa lakini.”

Nilimtazama mama na Kisha baba nikainuka pale nikisema β€œkila kitu ni sawa kabisa. Baba uwe na usiku mwema, mama yangu Nakupenda sana. Mimi niwaache sasa.”

Sikusubiri hata jibu, nikawa natoka huku nasikia mama anaita β€œRodricky, wewe Rodricky, Ricky mwanangu.”
Baba ana mwambia β€œmke wangu, Muache mtoto. Muache aende.”

Sijui waliendelea kuzungumza nini, mimi niliingia kwa garΔ± yangu, niliwasha garΔ± na kuanza safari ya kutoka pale nyumbani.

Share kwa ndugu na marafiki

WhatsApp
Facebook
Twitter

Chagua kipande kinachofuata

JOGGING MASTER FULL

SHEM MI NATAKA FULL

CHAGUO LA MOYO FULL