
LOML | Love Of My Life (60)

𝐋𝐎𝐌𝐋 (𝑳𝒐𝒗𝒆 𝒐𝒇 𝒎𝒚 𝒍𝒊𝒇𝒆) ❣️:60
Tukacheka Kisha nilisema “mke wangu, jitahidi kwa watu kuachana na simu sasa si unajua ugenini sio kitu kizuri.”
Alinitazama na kunishika akisema “am sorry babe, nisamehe sawa eneh haya hii hapa inakaa kWa mkoba.”
Nilitabasamu.
Nikawa naona mke wa Willy mwenyewe kavaa kwa heshima kapendeza anakuja upande wetu. Alipo tufikia alisema “Shemeji, karibuni sana ndani chakula kipo tayari.”
Nilitabasamu na kusema “Asante sana shemeji yako. Umejichosha sana kwaajili yetu.”
Alitabasamu na kusema “hapana kabisa shemeji karibu sana.”
Başı nilimtazama mke wangu na kumshika mkono na tulianza kuelekea ndani. Kama kawaida ndani sasa mezani wote pamoja.
Tulifurahi sana.
Tuliongea mengi na huku mke wangu akimpongeza mke wa Willy chakula kizuri nyumba nzuri na mambo Kama haya. Hakika tulifurahia siku yetu na mwisho tuliaga.
Tulipokuwa tunaondoka mke wangu aliniambia “nimeshangazwa na ukarimu wa watu hawa, nimejifunza mengi na nitajitahidi kufuata mengi hata kama sipendi sana kupika, kufua na mengi sasa naelewa kwanini hutaki kufuliwa. Mpenzi nitajitahidi nikufulie boksa zako, soksi zako, niandae meza. Nataka kuwa mwanamke mzuri.”
Nilimtazama na kusema “usijali mke wangu kama huwezi kufanya mtu mwingine anaweza kufanya ila walau ukasimamia. Unajua sio utumwa ni heshima na mapenzi. Mimi nakupenda tu Mke wangu.”
Mke wangu alitabasamu na kusema “nakupenda sana mume wangu na nashukuru kila siku najifunza mapya.”
Nilitabasamu na tuliendelea na safari ya kurudi nyumbani.
Tulifika nyumbani tukiwa na furaha sana. Nilipitiliza chumbani maana mke wangu alikuwa na vitu vyake na mama babuu. Nilifika chumbani na kujimwaga kitandani nikakumbuka nilivyo jidharirisha kwa dokta. Lakini ningefanya nini, walau najua mke wangu atakuwa salama na mwanangu tumboni hofu imeniondoka.

