LOML | Love Of My Life (114)

π‹πŽπŒπ‹ (𝑳𝒐𝒗𝒆 𝒐𝒇 π’Žπ’š π’π’Šπ’‡π’†) ❣️:114
Nikiwa nawaza hayo, simu yangu iliita tena. Niliitazama ile simu, alikuwa ni mama yangu. Nilishusha pumzi na kujituliza kwanza halafu ndiyo nilipokea. Nilisema kWa upole β€œmama!!”

Mama alinijibu β€œupo wapi wewe jamani, kwanini unakuwa hivi mwanangu?”
Nilishusha pumzi na kusema β€œnisamehe sana mama, nisamehe sana nakuomba. Nilitakiwa nirudi kazΔ±ni haraka sana.”

Mama alisema β€œmwanangu, ni sawa vyovyote vile. Lakini wewe ndiyo ulipata wa kushinda hapa haijalishi ni namna Gani mmegombana eenh. Akishapona mtakaa mzungumze kuliko hivi inaonyesha picha mbaya kwa watu unakuwaje lakini.”

Nilishindwa hata kumjibu mama yangu, mama aliendelea β€œhaya mwenzako jioni hii anaruhusiwa, unatufuata au inakuaje?”

Nilijikuta nasema β€œmama sitaki kumuona huyo mwanamke kwasasa, nataka kuwa mwenyewe, tafadhali nielewe mama.”

Mama alishusha pumzi na kusema β€œMungu wangu wewe mtoto umekuaje?. Huyu ni mke wako mwanangu, ni mkeo huyu. Unatupa mtihani wazazi wako hapa unafikiri tutafanyaje. Hatuwezi kumuacha binti arudi kwao na mimi nipo. Mimi na baba yako tunaondoka naye, halafu utamfuata unanielewa?”

Nililalamika na kusema β€œmamaaa!!, mamaaaa!! , Gabriella ana kwao mama, ana mama muache mimi nishachoka, muache aendee.”
Mama alikasirika, Alikata simu na kisha nilibaki naita β€œmama!!, mama!!, hello mama!!”

Mama alikuwa tayari amekata simu, na mimi nilikuwa nataka tu Gabriella aende kwao na sio kwetu. Roho ilikuwa inaniuma sana. Nilikuwa naumia.

Share kwa ndugu na marafiki

WhatsApp
Facebook
Twitter

Chagua kipande kinachofuata

LOML | Love Of My Life FULL

SHEMEJI UMECHOMEKA KWELI? FULL

TOBO LA PANYA FULL