
LOML | Love Of My Life (125)

๐๐๐๐ (๐ณ๐๐๐ ๐๐ ๐๐ ๐๐๐๐) โฃ๏ธ:125
Nakupenda sana mume wangu, nimekosa sana, nimekukosea mno, najuta mbele ya Mungu, padri wangu na familia pamoja na wewe mume wangu.
Nilikuwa mjinga na mpumbavu, lakini sipo tayari kukupoteza kwasababu nakupenda sana na najua siwezi kupata mwanaume kama wewe nakuomba sana.โ
Mama yangu alikuwa ananitazama akisema โmsamehe mwanangu, analia sana Muoneee huruma anaumwa.โ
Kฤฑla mtu akawa ananitazama nimsamehe, baba yangu alitaka hata nipigia magoti, nilijikuta nalia na kumuinua mke wangu na kumkumbatia.
Wao waliona kama nimesamehe Ila kwangu ilikuwa Bora ipite tu maana nimechoka sana. Walifurahi sana, wakapiga makofi. Amani ilitawala, nilimwambia mke wangu โacha kulia nimesamehe tuanze upya Ila sitavumilia tena ujinga huu.โ
Mke wangu alinitazama na kusema โnataka kuwa mke kwasasa hata kazฤฑ nitapumzika ili niwe karibu na wewe mume wangu.โ
Watu walizidi kufurahia. Tulibarikiwa, tukasali, tukala na nyumba ikawa na vicheko mpaka ile jioni wanaondoka wakitupongeza.
Tulibaki wawili na mimi nikaenda chumbani sina hata raha. Mke wangu alinifuata na kupiga tena magoti na kusema โnajua una hasฤฑra na mimi, nakuelewa mume wangu Ila nipo tayari kuwa mke wako tafadhali nipokee.โ
Nilimtazama na kumuuliza โUpo tayari kuzungumza na mtu wa tiba ya akili, mnasihi.โ
Alinitazama na Kisha aliniuliza โkwanini unasema hivyo mume wangu?โ
Nikamuuliza โulipanga kuniambia lini kuhusu wewe na mama yako?โ
Aliinamisha kichwa na kรผsema โnisamehe mume wangu.Sikutaka kukusumbua. Nipo tayari kufanya lolote niwe Bora.โ
Nilimwambia โatakuwa anakuja hapa, Hakuna kwenda kazini. Hatutafanya lolote mpaka nijiridhishe tabia zako na Baada ya hapo nitatimiza ahadi yangu ya Paris ili tukaanze upya kabisa.โ

