LOML | Love Of My Life (125)

π‹πŽπŒπ‹ (𝑳𝒐𝒗𝒆 𝒐𝒇 π’Žπ’š π’π’Šπ’‡π’†) ❣️:125
Nakupenda sana mume wangu, nimekosa sana, nimekukosea mno, najuta mbele ya Mungu, padri wangu na familia pamoja na wewe mume wangu.

Nilikuwa mjinga na mpumbavu, lakini sipo tayari kukupoteza kwasababu nakupenda sana na najua siwezi kupata mwanaume kama wewe nakuomba sana.”

Mama yangu alikuwa ananitazama akisema β€œmsamehe mwanangu, analia sana Muoneee huruma anaumwa.”

KΔ±la mtu akawa ananitazama nimsamehe, baba yangu alitaka hata nipigia magoti, nilijikuta nalia na kumuinua mke wangu na kumkumbatia.

Wao waliona kama nimesamehe Ila kwangu ilikuwa Bora ipite tu maana nimechoka sana. Walifurahi sana, wakapiga makofi. Amani ilitawala, nilimwambia mke wangu β€œacha kulia nimesamehe tuanze upya Ila sitavumilia tena ujinga huu.”

Mke wangu alinitazama na kusema β€œnataka kuwa mke kwasasa hata kazΔ± nitapumzika ili niwe karibu na wewe mume wangu.”

Watu walizidi kufurahia. Tulibarikiwa, tukasali, tukala na nyumba ikawa na vicheko mpaka ile jioni wanaondoka wakitupongeza.

Tulibaki wawili na mimi nikaenda chumbani sina hata raha. Mke wangu alinifuata na kupiga tena magoti na kusema β€œnajua una hasΔ±ra na mimi, nakuelewa mume wangu Ila nipo tayari kuwa mke wako tafadhali nipokee.”

Nilimtazama na kumuuliza β€œUpo tayari kuzungumza na mtu wa tiba ya akili, mnasihi.”
Alinitazama na Kisha aliniuliza β€œkwanini unasema hivyo mume wangu?”
Nikamuuliza β€œulipanga kuniambia lini kuhusu wewe na mama yako?”

Aliinamisha kichwa na kΓΌsema β€œnisamehe mume wangu.Sikutaka kukusumbua. Nipo tayari kufanya lolote niwe Bora.”
Nilimwambia β€œatakuwa anakuja hapa, Hakuna kwenda kazini. Hatutafanya lolote mpaka nijiridhishe tabia zako na Baada ya hapo nitatimiza ahadi yangu ya Paris ili tukaanze upya kabisa.”

Share kwa ndugu na marafiki

WhatsApp
Facebook
Twitter

Chagua kipande kinachofuata

BIKIRA YA BIBI HARUSI FULL

UKO HOME NIJE FULL

TOBO LA PANYA FULL