LOML | Love Of My Life (132)

𝐋𝐎𝐌𝐋 (𝑳𝒐𝒗𝒆 𝒐𝒇 𝒎𝒚 𝒍𝒊𝒇𝒆) ❣️:132
Natamani hata nikuambie kuwa simu ni maisha ya mtu, simu yako Ina kitu gani, simu yako Ina jambo gani? Hakikisha hutumii simu yako kuharibu maisha yako au ya mtu mwingine.

Mikononi mwanangu sikuwa na uwezo wa kushika hata simu kwa muda mrefu kabisa. Kwasababu nilikuwa natetemeka sana. Hata nilicho kiona sikuwa naogopa sana kwasababu ndiyo halisi alivyo Gabby.

Hapo sasa niliona namna huwa wanachat mke wangu na Giana. Mara zote huwa najua kuwa ni marafiki nisifuatilie mambo ya kike Kumbe kuna zaidi.

Halafu sasa walivyo romantic hata kuna mahali Giana anasema “baby nakumiss sana unajua. Naona nowdays hutaki tena maana ni wewe na mumeo unasahau kabisa mapenzi yetu hayapaswi kuisha.”


Na mke wangu anamjibu “baby wangu, Acha ujinga Nani anaweza kunipa raha kama unazonipa Nakupenda mpaka nachanganyikiwa mwenzako, hapa nilipo namiss penzi lako hata mtu anifanyie nini hakuna aliyewahi nifikisha unapo nifikisha, nakupenda G wangu.”

Na Giana na yeye anajibu kimahaba, hizo I miss you, Hizo baby usiumwe tafadhali naumwa zaidi, nakupenda mpenzi wangu mzuri, kipipi changu, na mengine mengi, picha za wao wakigusanisha ulimi, picha wakishikana matiti na picha za mahaba kWa chat zao ni za kutosha sana.

Hawa ni wapenzi wa muda mrefu sana. Nililia sana kuoa mwanamke ambaye hata shetani anashangaa nimepata wapi mwanamke kama huyu.

Nililia sana nikiwa hapa kanisani. Na nilitumia muda mwingi sana hapa hata nilivyokuwa nazidi kukaa hapa ndiyo hali yangu ilikuwa inazidi kuwa mbaya.

Share kwa ndugu na marafiki

WhatsApp
Facebook
Twitter

Chagua kipande kinachofuata