LOML | Love Of My Life (160)

π‹πŽπŒπ‹ (𝑳𝒐𝒗𝒆 𝒐𝒇 π’Žπ’š π’π’Šπ’‡π’†) ❣️:160
Umepata nguvu wapi ya kuja kusimama mbele yangu na kulia kama hakuna kitu kimetokea. Sijakufanya kitu kibaya, sijawahi kukuumiza kama nilivyo paswa kufanya.

Tangu awali nakuoa sikukupenda, kila mtu anajua hilo lakini nilipata nguvy ya kukupa nafasi kama mke nikakupenda na kukujali na ukafanya ninj Gabby.

Haya yote hakuna hata una stahili kwasababu wewe unatakiwa kuumia kama hutokuja kuumia tena. Pengine hujaelewa, maumivu yako hayanizuii kuishi, kufanya maisha mengine unajua kwanini, kwasababu maumivu yanayotoka kwa mwanamke ambaye hana akili hayadumu kwa mwanaume mwenye upendo na akili timamu.

Nakuchukia, nachukia siku ambayo ulikuja kwenye maisha yangu, nachukia kukuona, karibu na ndugu zangu wala mbele yangu. Sikupendi, sikupendi na ndoa yangu mimi na wewe sio kuisha Imekufa kabisa. Gabby hata kichaa hawezi kuwa na mke mshenzi kama wewe.”

Gabby alikuwa analia akisema β€œRicky pleaseee!!”
Huku mama akisema β€œinatosha!!, nini shida kwani ninyi watoto.Eenh Ricky nini kinaendelea. Kwanini maneno makali hivi kwa mkeo, kwani nyie watoto hamuwezi kuelewana hata kidogo kwanini?”

Nilimtazama Gabby na kusema β€œtokaaaaa!!, tokaaa!!, tokaaaaaaa!!, tokaaaaaaaaaaaaaa!!!”
Gabby alinitazama analia na kufungua mlango kuelekea nje huku mama akinituliza na kusema β€œunaumwa unajua, kwanini unafanya hivi lakinu eenh!!”

Mimi nilikuwa nalia kwa maumivu. Mama alinikumbatia na kuniambia β€œmwanangy tafadhali tulia, tulia tafadhali.”

Nilishusha pumzi nikisema β€œmama nahitaji kuwa mwenyewe nakuomba.”
Mama alinitazama na kusema β€œkivipi, umelala hapa siku mbili bila mama wala baba yako. Haitoshi wewe ni mume wa mtu mbele yangu una mwambia mwanamke mwingine una mpenda sana.

Share kwa ndugu na marafiki

WhatsApp
Facebook
Twitter

Chagua kipande kinachofuata

BIKIRA YA BIBI HARUSI FULL

UKO HOME NIJE FULL

BIOLOGY TEACHER FULL