LOML | Love Of My Life (163)

π‹πŽπŒπ‹ (𝑳𝒐𝒗𝒆 𝒐𝒇 π’Žπ’š π’π’Šπ’‡π’†) ❣️:163
Mama alibeba mkoba wake kwa hasira na kutoka. Nilibaki nimekasirika sana. Nilikasirika kwa maneno ya mama yangu. Alivyo zungumza kuhusu Pina, na namna anataka mambo yawe.

Lakini baada ya kukumbuka maneno ya Pina. Busu lake nilitabasamu. Na wakati huo dokta alikuwa anaingia. Niliendelea kutabasamu hata akasema β€œnaona una furaha sana.”

Nilitabasamu na kusema β€œmaisha yananipa sababu ya kutabasamu kwa mara nyingine.”

Dokta alitabasamu na kisha aliendelea na kazi yake na kusema β€œulikuwa unaendelea vizuri, kwasasa naona hali yako imebadilika tena. Sikia nikuambie kitu Rodricky, unatakiwa kutulia kabisa ili hali hii ikae sawa usifanye masihara tafadhali sio nzuri.”

Nilivuta pumzi na kusema β€œnimekuelewa tafadhali, nitakuwa makini. Naomba ukitoka hapo niitie Pina na Willy.”
Dokta alinitazama na kusema β€œPina sijamuona. Willy yupo.”
Nilishtuka, huku moyoni nikijiuliza β€œina maana ameondoka?”

Nilitamani kujua hili kutoka kwa Willy. Dokta alimaliza mambo yake na kisha alitoka. Alipotoka tu haukupita muda sana Willy aliingia ana tabasamu. Sikuacha hata amalize kutabasamu nikamuuliza β€œKaka Pina ameondoka?”

Willy alinitazama na kusema β€œkaka kile chuma umetoa wapi?”
Nilimtazama na kusema β€œuna maana gani?”
Aliniambia β€œniahidi utanisimulia kila kitu kuhusu yeye. Sio poa, amenyooka hivi, haogopi na hapo ni haoni lakini Mungu wangu!!, Mungu wangu!!!”
Nikamuuliza Willy β€œacha mafumbo, niambie nini kimetokea?”
Alishusha pumzi na kusema β€œbaada ya kutoka hapa, alionekana hana raha hata nikamuuliza kama yupo sawa. Alinijibu tu nisijali yupo sawa.

Baada ya muda mkeo alitoka analia, na moja kwa moja alikuja mpaka kwa Pina. Sasa si unajua Pina haoni, mkeo alianza kupiga kelele zake na tambo nyingi akimtaka Pina akae mbali na wewe.

Share kwa ndugu na marafiki

WhatsApp
Facebook
Twitter

Chagua kipande kinachofuata

BIKIRA YA BIBI HARUSI FULL

SHEMEJI UMECHOMEKA KWELI? FULL

UKO HOME NIJE FULL

UTAMU WA JAMILA FULL