LOML | Love Of My Life (165)

π‹πŽπŒπ‹ (𝑳𝒐𝒗𝒆 𝒐𝒇 π’Žπ’š π’π’Šπ’‡π’†) ❣️:165
Maisha ni fumbo, na mafanikio ni siri ya Mungu yeye mwenyewe.Mfungua mafumbo hayo ni Mungu peke yake, anayejua uchungu wa kukosa na makosa ya kupata.

Kwa bahati mbaya huna akili hiyo, na upo hapa unasema mimi kipofu na wewe mwenye macho umeshindwa kuona uzuri wa mwanaume mzuri kama Rodricky, hakutaki tena kwasababu wewe ni mchafu, unanuka, unatia kinyaa.

Halafu unataka kuzungumzia hadhi na heshima. Ulishindwa kuona heshima anayokupa Ricky, unataka yangu mimi. Sikia nitakufundisha namna wanaume wenye moyo mzuri, wanaume wazuri na wanaojua kupenda kama Ricky wanapaswa kuheshimiwa.

Sina macho ila nitatumia macho ya Ricky kukufanya uone. Simuachi, sikai naye mbali, ndiyo kwanza tunaanza, na wewe mwenye macho na kila kitu, utapaswa ukae vizuri utazame kwa uzuri zaidi kuona namna mapenzi na mpenzi uliyemuumiza yalivyo.

Umepoteza Gabby, tena umepoteza kitu cha thamani sana na kwa bahati mbaya maskini kama sisi sio wepesi kuachia hatima tamu kama hizi. He is my forutune(Ricky ni bahati yangu), he is my fate (ni hatima yangu), he is my smiley (ni tabasamu langu, Upo hapo Gabby!!!, relax!!”

Niliona Gabby akichukia, alimnasa kibao Pina alikasirika na kusema β€œkwa bahati mbaya, maumivu kwenye maisha yangu yalinifundisha mengi sana.”

Alimtia vibao viwili mfululizo yaani mashavu yote huku na huku.Nikasikia Willy anasema β€œmnachanganyikiwa hamuonu hapa ni hospitali.”

Pina anatabasamu, na video iliishia hapa. Nilishangaa nikisema β€œMungu ina maana Pina sio mnyonge namna hii. Sikutegemea haya unajua. Amesema mimi ni bahati yake, hatima yake na tabasamu lake.

Share kwa ndugu na marafiki

WhatsApp
Facebook
Twitter

Chagua kipande kinachofuata

JOGGING MASTER FULL

CHAGUO LA MOYO FULL

UTAMU WA JAMILA FULL