LOML | Love Of My Life (168)

𝐋𝐎𝐌𝐋 (𝑳𝒐𝒗𝒆 𝒐𝒇 𝒎𝒚 𝒍𝒊𝒇𝒆) ❣️:168
Pina alisema “nooo!! Nooo!!, noo!! Ulifanya kitu hata Mungu anapenda tufanye. Ulisamehe na kuendelea na maisha. Yule mwanamke ndiyo mjinga sana, yeye ndiyo kipofu haoni, kabisa yaani alishindwa kupokea nafasi ulizompatia.”

Nilitabasamu na kusema “uwepo wako pembeni yangu ni zaidi ya kila kitu Pina. Wewe ni mwanamke ambaye unanifanya nijisikie vizuri sana ndani ya moyo wangu. Unanipa sababu ya kuwa imara, unanijali sana na kunipenda.

Wewe ni zadii ya bahati kwangu. Pina wewe ni Hatima yangu you are my Fate, my fortune and my smiley, ninakupenda haki ya Mungu. Sitamani kukupoteza. Nitafanya kila kitu uwe na mimi, ubaki hapa na mimi.

Tafadhali niambie, unanipenda?, sahau kuhusu maumivu, kila kitu kwasababu mimi sijali chochote ninachojali ni kitu kimoja tu unanipenda?”
Pina aliniuliza “huogopi kuumia wakati bado una maumivu?”

Nilimtazama na kusema “kama yanatoka kwako sijali, sijali kwasababu yatatoka kwa mtu ninaye mpenda sana.”
Pina alitabasamu na kusema “Willy huyo amekuambia kuhusu Fortune, smiley na fate eenh.”

Nilitabasamu na kisha alinigeukia, akaniambia kwa upole “tangu siku ya kwanza nimekuona kanisani, nilijua hili litatokea. Nilipo sikia sauti yako, ndani ya moyo wangu nilijihisi tofauti sana.

Nilifanya juhudi za kukaa mbali na wewe lakini hisia zimeshindwa kabisa. Kelele za nakupenda, nakupenda, nakupenda zilikuwa ni nyingi ila ningefanya nini na wewe ni mume wa mtu Ricky.

Share kwa ndugu na marafiki

WhatsApp
Facebook
Twitter

Chagua kipande kinachofuata