
LOML | Love Of My Life (172)

๐๐๐๐ (๐ณ๐๐๐ ๐๐ ๐๐ ๐๐๐๐) โฃ๏ธ:172
Nilimtazama Willy na kusema โMoyo umechoka sana, Nipo hapa kwasababu ya mambo yake ya ajabu. Willy kwa alicho nifanyia hata mbinguni sidhani kama bado tupo kwa orodha ya wanandoa. Ndoa yetu imekufa kabisa.
Nikitoka hapa, kabla ya kwenda popote ni kanisani kufuatilia taraka. Tena natamani iwe haraka sana na nifanikiwe kwenye hili. Kusema ukweli sitamani hata kukumbuka mimi ni mume wake au nimewahi muoa. Ni mshenzi sana.โ
Willy alishangaa na kuuliza โni serious namna hiyo?โ
Nilisema kwa upole โnashangaa hata ujasiri huo ametoa wapi kuonekana na kujiliza kwangu. Alipaswa kuona aibu, na kujificha maisha yote. Kaka ipo siku nitakuelezea haya kwasasa acha nipumzike tu sitaki kuteseka lakini niambie vipi Pina?โ
Willy alitabasamu na kusema โNimempenda.โ
Nilimtazama na kusema โongea vizuri kaka, umempenda aje sasa shemeji yako yule.โ
Willy alicheka akisema โumekamatika kaka, toto zuri lile aiseee, halafu haachi kunishangaza. Mmenipa raha sana.โ
Nilitabasamu nikisema โnitumie ile video.โ
Akacheka akisema โnilijua tu lazima, lazimaaa!!โ
Tulicheka, na mwisho wa yote alinitumia video, akaniaga na kuondoka zake nilibaki chumbani peke yangu. Nilikuwa namuwaza tu Pina wangu, na kutabasamu hata nikapitiwa na usingizi.
Ulipita muda kidogo tu, baba yangu aliingia na aliniamsha. Nilipoamka baba yangu alinikumbatia kwa furaha sana na kusema โmwanangu una shida gani, unapata tatizo husemi mpaka unalazwa umenyamaza tu, au unatuchukia wazazi wako maana sijakuelewa. Hata mimi msiri wako, eenh kijana wangu. Unajua wazi mimi bila wewe sio kitu. Wewe ndiyo nguvu yangu na sasa unataka nife au wewe ufe nilie mpaka udongo unimeze na mimi.โ

