LOML | Love Of My Life (176)

π‹πŽπŒπ‹ (𝑳𝒐𝒗𝒆 𝒐𝒇 π’Žπ’š π’π’Šπ’‡π’†) ❣️:176
Baba alitabasamu akinifuta machozi huku uso wake ukionekana kuumia akisema β€œmwanaume anajikaza, mwanaume anafanya maamuzi.Mwanaume yeyote yule ni mtu wa msimamo.

Usijali kuhusu mama yako, najua unaelewa wanawake walivyo but i promise you that, i will make her understands kila kinachoendelea. Najua kwasasa ni ngumu, wacha upone halafu mchakato wa taraka na nitakusaidia mwanangu.

Lakini sasa tuzungumze kuhusu huyu mwanamke mpya nataka kujua ni nani?, unampenda ?, wapi ametokea mbona ghafla hivi mwanangu..”

Nilitabasamu na kusema β€œbaba she is very beutiful girl, ana moyo mzuri, ni rafiki yangu. Hatujafahamiana muda mrefu ila ananielewa kuliko mtu yeyote.

Ana mjua Mungu vizuri na msaada wake umechangia sana mimi kufika hapa leo hii. Ni mtu mzuri sana baba. Nilimuona mara ya kwanza siku ya ndoa yangu kanisani?”
Baba alisema β€œwacha weee, pale unakutana na soulmate ukishaoa.”

Nilicheka sana na kusema β€œkabisa baba , lakini niliheshimu ndoa yangu, kwasababu sikutaka kukuangusha.”
Baba alitabasamu na kusema β€œnakuelewa sana mwanangu, nakuelewa.”

Wakati tunazungumza mara mlango ulifunguliwa, alikuwa ni Pina amebeba kifungashio. Alikuwa anatabasamu na mimi nilikuwa natabasamu nikimwambia baba β€œni yeye baba!!, ni yeye!!”

Share kwa ndugu na marafiki

WhatsApp
Facebook
Twitter

Chagua kipande kinachofuata

JOGGING MASTER FULL

SIMULIZI YA INGIZA FULL