LOML | Love Of My Life (190)

𝐋𝐎𝐌𝐋 (𝑳𝒐𝒗𝒆 𝒐𝒇 𝒎𝒚 𝒍𝒊𝒇𝒆) ❣️:190
Başı yangu aliniambia mtoto atajisiadia niandae chombo tu hata kama ni ndoo. Başı na mimi nilifanya hivyo kweli saa moja, mtoto wangu alianza kuhara, kwenye ile ndoo namuweka.

Mtoto analia, cha ajabu mtoto wangu alikuwa Ana hata uchafu sana, usaha wa kutisha na kunuka ni Kama umeoza sana. Nilikuwa nalia huku nasema “Asante Yesu, Asante Yesu.”

Bibi yangu alinikuta kwa hali hiyo, nilipomuona bibi yangu, sikumsalimia hata nilibeba kile choo na kumwambia “nakuja bibi angalia mtoto.”
Niliondoka kwa pikipiki mpaka huko, nilipofika palikuwa kimya sana mida ya saa 3.

Nilisikia kama watu wanazungumza chumbani. Nilinyata na kusikia mama anasema “nilikuambia, Yule mwanamke hakufai ulibisha unaona sasa anatusumbua eenh, sasa hivi hatupati yeye wala mtoto.

Ungebaki na mkeo wa kwanza tu. Sasa unafikiri tunafanyaje imeshakuwa ngumu.”
Mume wangu anasema “hawezi kutushinda huyu, na lazıma anyooke hawezi kuingilia mambo yetu kabisa.”

Niliziba mdomo, Ina maana huyu mwanaume hakunipenda kuna kitu alihitaji kwangu, kunitumia au kuniua. Ni wachawi au washirikina hapo ndiyo sielewi. Niligonga mlango, mama alifungua akiwa na upande wa kanga.

Aliponiona alishtuka, nilimtazama na kusema “nimeleta uchafu wenu. Na nimekuja kukuonya kuwa mtoto wangu akifa ni wewe na kijana wako mmeua na kila mtu atajua hilo. Mtoto wangu akifa, mtamla nyama. Na kuanzia sasa mkae mbali na sisi. Kamwe sijaingilia mambo yenu Bali ninyi na Hakuna kitu mtanifanya.”

Huyu mama alinitazama akauliza “unazungumzia nini?”
Nilimtazama kwa hasıra sana na kuondoka zangu.

Share kwa ndugu na marafiki

WhatsApp
Facebook
Twitter

Chagua kipande kinachofuata