LOML | Love Of My Life (202)

๐‹๐Ž๐Œ๐‹ (๐‘ณ๐’๐’—๐’† ๐’๐’‡ ๐’Ž๐’š ๐’๐’Š๐’‡๐’†) โฃ๏ธ:202
Nilitabasamu na kusema โ€œsana Pina, sana na pamependeza.โ€
Pina alitabasamu na kusema โ€œwaoooo!!, ni pazuri sana, eenh niambie pamendeza sana.โ€
Nilitabasamu na kusema โ€œsana Mpenzi.โ€

Alianza kama kunipapasa, hapa ndiyo nikatoa fimbo ambayo nilikuwa nimeishikilia mimi na kusema โ€œhii ndiyo zawadi yako.โ€

Nilimpatia mkononi na kusema โ€œmimi nikiwepo huna sababu ya kutumia. Nikiwa mbali na wewe utatumia fimbo hii. Ni nzuri sana, Ina fanana sana na wewe, halafu Ina ngโ€™ara vizuri sana.โ€

Pina ni kama sijui nimempa kitu gani kwa furaha ile. Alikuwa anaishika shika ile fimbo akisema โ€œbaby ni nzuri sana, tazama inavyo teleza. Ni nzuri sana yaani, nimefurahi sana.

Natamani uone namna nimefurahi Mungu wangu, Ricky umenikumbuka jamani. Sistahili this love, baby wewe ni mwanaume unayejali sana. Tazama, ona ilivyo nzuri.โ€

Nilimsogelea na kusema โ€œnitafanya kila kitu kuhakikisha unakuwa na hii furaha maisha yako yote. Utakuwa na furaha hii hii. Karibu sana Pina.โ€

Pina alinikumbatia kwa nguvu, hata nilimbeba na kuanza kuzunguka naye, Kisha Tulijikuta tumeangukia kitandani. Alikuwa juu yangu, na mimi nilikuwa chini, nikawa namtazama namna alivyo mzuri, alikuwa ametulia tu.

Kisha nilimbusu taratibu midomo yake mizuri, alinibusu pia na Kisha tulijikuta tunacheka. Tulicheka huku Pina alisema โ€œmimi ni mzito sana, nilisahau mgonjwa wangu hana nguvu kabisaa.โ€

Nilicheka nikisema โ€œhuna akili ujue, utakuja kuniua mimi.โ€

Share kwa ndugu na marafiki

WhatsApp
Facebook
Twitter

Chagua kipande kinachofuata