
LOML | Love Of My Life (205)

๐๐๐๐ (๐ณ๐๐๐ ๐๐ ๐๐ ๐๐๐๐) โฃ๏ธ:205
Pina alitabasamu na Kisha alisema โmama!!, tafadhali mimi naomba niite tu Pina!!, ndiyo napenda zaidi.โ
Nilitabasamu na Kisha nilisema โAu muite mama Ricky hapo vipi si jina zuri zaidi?โ
Tulitazamana na kujikuta tunacheka sana. tulicheka huku Pina akisema โhuna akili kabisa, huna akili.โ
Wakati anasema hivyo mlango ulikuwa unagongwa, mama Babuu alienda kufungua. Alikuwa ni baba yangu, baba alipofika alisema โkumbe mimi mkulima mzuri, mwanangu share yangu ipo hapo.โ
Nilicheka nikisema โbaba huwezi kukosa chakula ukiwa kwa mwanao.โ
Baba alitabasamu na nilisimama kumkumbatia, Pina alisimama pia na kusema โShikamoo baba!!โ
Baba aliitikia na kusema โnimefurahi sana kukuona hapa binti yangu.โ
Pina alitabasamu, baba akaniuliza maendeleo yangu basi nikamuelekeza namna ninajisikia wakati mwingine sawa na wakati mwingine ovyo.
Na niliongeza โYote kwa yote Namshukuru sana Pina. Amekuwa msaada sana kwangu. Yupo na mimi kila wakati kunikumbusha dawa, namna ya kujitunza na kula.โ
Baba alitabasamu, nilimtazama na kusema โeenh mama anaendeleaje?โ
Baba alisema โunajua mama yako, bado anaona Yule mchawi ndiyo mwanamke mzuri. Laiti angejua kuwa ni mashine ile ya kusaga na kukoboa angekaa mbali kabisa.โ
Tulijikuta tunatazamana na kucheka sana, baba alisema โmnisamehe wanangu, nimechukia sana.โ
Baba alinitazama na kusema โhapa ninavyo kuambia mama yako ameenda kwao Gabby. Nasikia Gabby kawaelezea kwao kuwa una mpenzi mpya na humtaki yeye kฤฑsa huyo mpenzi.โ
Mimi nilimtazama Pina, akawa anatabasamu tu. Mama Babuu yeye alikuwa ana andaa chakula cha baba. Kisha alisema โnashukuru sana kwa chakula kizuri Pina. Ubarikiwe Ila uzingatie tulivyo zungumza.โ

