LOML | Love Of My Life (216)

𝐋𝐎𝐌𝐋 (𝑳𝒐𝒗𝒆 𝒐𝒇 𝒎𝒚 𝒍𝒊𝒇𝒆) ❣️:216
Alitabasamu na kusema “Nakupenda My Fortune.”
Nilitamani nimbusu tena Ila sasa bibi pale, nikamtania “Natamani goodbye kiss Ila sasa yupo na sisi.”
Alitabasamu, akanibusu paji La uso ile ya kushtiza akisema “goodnight handsome.”Akaondoka zake haraka haraka.
Nilibaki natabasamu tu. Na Kisha nikaingia zangu ndani ya gari na kuanza safari ya kuondoka zangu nikiwa Nakumbuka ujinga wa Pina wangu nacheka tu.

Başı nikiwa ndani ya gari, simu ya Gabby inaonekana kuna namba ilikuwa inapiga sana. Nilikuwa natazama tu, huku ndani yangu nilikuambia “lazıma nimfuate Giana na yeye ndiye atapeleka hii simu kwa mwenyewe. Nataka kuzungumza naye pia. “

Nikamuelezea dereva mahali nataka kwenda. Başı ile namba ikawa inaendelea kusumbua. Nilijikuta ndani yangu natamani kujua huyu mtu ni nani tena mbona hii ni line mpya mke wangu Baada ya ile ugomvi akibadilika akanunua na line mpya Kumbe Hana lolote. Huyu mwenye hii namba ni nani tena.

Nikaingia kwa simu yake, nilijikuta nacheka tu. Sio kwamba Giana ni ana msaliti mumewe na Gabby. Bali Mumewe pia anamsaliti mkewe na Gabby. Ni wapenzi wazuri sana.

Tena wanaitana shem darling. Unajua tena badala ya kuumia unacheka. Ukiona huyo mume wa Giana anavyo msifia Gabby, anamtumia mpaka picha za sehemu zake, Gabby na yeye anamsifia kwa vile anavyo mpa raha.

Nilisoma tu simu nikisema “Nipo sahihi, Gabby ni jini.Gabby ni shetani, anahitaji msaada mkubwa huyu sio mwanamke wa maisha yangu mimi, ni pasua kichwa.

Anamfanyia haya hata rafiki yake ambaye ni mpenzi wake. Ngumu kuitamka Ila ndiyo ukweli Gabby na Giana ni wapenzi na haifutiki hii. Ndiyo ukweli wenyewe.

Share kwa ndugu na marafiki

WhatsApp
Facebook
Twitter

Chagua kipande kinachofuata