LOML | Love Of My Life (247)

๐‹๐Ž๐Œ๐‹ (๐‘ณ๐’๐’—๐’† ๐’๐’‡ ๐’Ž๐’š ๐’๐’Š๐’‡๐’†) โฃ๏ธ: 247
Hapa sahau kuhusu Pina wa zamani, Pina wa sasa ni mzuri zaidi, anawaka, na vile tunapaka mafuta mazuri utatuambia nini. Tumependeza mno, ni mwanamke wa hadhi yangu kabisa.

Niliendesha gari mpaka nyumbani kwao Pina. Hapa sio kama zamani. Ingawa Pina Mara nyingi nakuwa naye kwangu lakini hasahau kwao. Nilifanya marekebisho makubwa kupaka rangi, kuweka tiles mpya na kuwabadilishia madirisha.

Na vitu vya ndani kwa namna niliweza. Nje nikawajengea jiko na mahitaji yote muhimu ili mradi tu wajisikie vizuri kuwa hapo.

ลžam na yeye ni shule na nalipia vizuri kabisa bila wasiwasi kabisa na anafurahia maisha yake ya shule mpya. Kiufupi nilitamani hata kama sio sana basi walau maisha ninayoishi mimi na wao waishi hata kidogo tu.

Pina alifurahia sana, tuliagana na nilirudi nyumbani. BaลŸฤฑ nakumbuka nilipofika nyumbani simu yangu iliita, alikuwa ni mama yangu. Nilipokea na kumsalimia mama.

Mama yangu aliniambia โ€œmwanangu, sikuelewi unajua. Ina maana ndiyo huyo kipofu wako amekukataza hata kuzungumza na mimi. Nasikia umenunua eneo hunambii chochote. Hivi una shida gani wewe?โ€

Nilijikaza sana, nilitamani hata nisimjibu kabisa nilishindwa, nilimjibu mama yangu โ€œMama, unanikera sana, sikuhizi una roho mbaya sana.โ€
Halafu nilikata simu.

Hapo ujumbe uliingia โ€œunanikatia simu kisa kumwambia ukweli mwanangu. Umekua vibaya au sio.โ€
Nilichukua ule ujumbe na kumtumia baba yangu. Baba alipiga muda uleule na kusema โ€œkumekucha ni nini tena?โ€

Nilimwambia baba kWa hasira โ€œSijui mama ana tatizo gani, hawezi kumuongelea Pina kwa mazuri. Kฤฑla akipiga lazima tugombane. Baba mimi ni mtu mzima, nachoka sasa, nitapoteza uvumilivu kabisa kwake. โ€œ

Baba alisema kwa upole โ€œpole sana mwanangu, Pole sana. Nakuomba usiendelee kugombana naye mimi nitazingumza naye na kฤฑla kitu kitakuwa sawa kabisa.โ€

Nilisema kWa upole โ€œfanya hivyo baba, mimi nachoka, nashindwa kuvumilia kunitukania mwanamke wangu na kumsema vibaya kฤฑla akipata nafasi ya kuzungumza na mimi. Mama ana kera sana.โ€

Nilikata simu, hata furaha yangu mama anataka tu kunikwaza ili mradi. Nashukuru ninaye baba yeye ananituliza sana.

Mama utadhani alizaliwa na utajiri, anakuwa sio muelewa kuwa hata yeye kesho na kesho kutwa kilichompata Pina kinaweza nipata hata mimi.

Anapata wapi ujasiri wa kuwa na roho ngumu namna hii. Ni mama yangu lakini sikupenda kabisa tabia yake kwa mwanamke wangu ambaye mimi ninampenda sana.

Nakumbuka siku mbili baadaye nilitembelewa na mgeni ofisini kwangu. Alikuwa ni mume wa Giana.

Nilimkaribisha, na yeye aliniambia โ€œkaka nipo hapa kukushukuru kwa upendo wako, kwa hekima na kuokoa ndoa yangu. Nilikuwa sio kijana mzuri kwa mke wangu, pengine ulichokiona ni kidogo sana.

Lakini Kiukweli nilikuwa nipo vibaya zaidi. Baada ya yale maneno siku ile nilitafakari sana na kujiuliza ninakosa nini nikitulia na mke wangu na kutunza familia yangu.

Niliacha kabisa habari za kuruka huku na kule. Nilipata muda wa kukaa na kuzungumza na mke wangu. Tuliamua kufanya maisha yetu kuwa mazuri.

Tangu hapo kaka, Mungu ametubariki sana, maisha yamekuwa rahisi kuliko awali. Wewe ni kama Malaika alikutumia kuja kuniamsha usingizini. Ni kama nilipitia yale nifahamiane na wewe.

Share kwa ndugu na marafiki

WhatsApp
Facebook
Twitter

Chagua kipande kinachofuata

SHEMEJI UMECHOMEKA KWELI? FULL

UTAMU WA JAMILA FULL

LOML | Love Of My Life FULL

CONNECTION YA BALTASAR FULL