LOML | Love Of My Life (116)

π‹πŽπŒπ‹ (𝑳𝒐𝒗𝒆 𝒐𝒇 π’Žπ’š π’π’Šπ’‡π’†) ❣️:116
Najua watu ni wazuri sana kuficha hadithi zao chafu, watu wengi sana kwenye vitabu vyao wanapenda kuachana kurasa mbaya na kubaki na zile nzuri tu kitu ambacho sio kizuri kwasababu ukweli ndiyo kitu pekee umuweke mtu kwenye maisha yake.

Mfahamu mtu unaenda kufunga naye ndoa, hata kama kwa kidogo tu. Na kamwe usipuuze ishara yoyote ile mbaya kwenye mahusiano yako. Zingatia ishara hizo. Zifanyie na uanze kuzifuatilia.

Zina maana kwenye maisha yako, upendo usikupumbaze, usiingie kwenye ndoa kwasababu tu unataka kuoa.Zaidi ni Mungu tu ndiyo anajua.

Huko awali nilisema β€œhakuna kitu kinatokea kwenye maisha yako kama bahati mbaya. KΔ±la kitu kimetokea kwasababu kilikuwa lazima kitokee.”

Nilikuwa naumia na mengi sana hapa, nilikuwa najisikia vibaya ndani ya moyo wangu. Nilikuwa nakumbuka nyakati tukiwa na furaha, namna alivyo mwanamke huku. Lakini nikikumbuka namna nimeumia nalia sana, naumia sana.

Kwenye haya maisha yako ya kΔ±la sΔ±ku, unaweza kumsamahe mtu yeyote Yule aliyekukukosea. Haijalishi kosa gani, haijalishi kamwe usisahau namna amekufanya ujisikie ndani ya moyo wako.Namna unajisikia ndiyo namna hiyohiyo itakufanya uweke mipaka kati yako na huyo mtu. Msamahe lakini usiache kusahau namna unajisikia.”

Nilikuwa nimekaa tu hapa nawaza hili na lile, lile na hili. Ilinichukua muda mrefu sana. Lakini ningefanya nini sasa zaidi ya kuendelea kutafakari maisha yanavyo nipeleka.

Ujumbe uliingia kwa simu yangu. Nilishika simu na kufungua ujumbe ule, alikuwa ni Gabriella na Aliandika β€œMume wangu, nisamehe tafadhali πŸ’”πŸ˜­, nitakufa bila wewe mume wangu, nitakufa mpenzi. Nitawezaje kuishi bila wewe.

Uwepo wako kwenye maisha yangu unanivusha na mengi sana. Kukosekana kwako kunasababisha shimo kubwa na refu sana ndani ya moyo wanguπŸ’”, mimi ni mjinga sana, nimepoteza, nimeharibu maisha yangu kwa kumpoteza mwanaume mzuri sana.

Mume wangu ninakuomba tafadhali, najua sina zuri La kufanya unikumbuke. Niamini mapenzi yangu kwako ni kweli kabisa. NISAMEHEπŸ˜­πŸ’”πŸ’”, bedo❣️ nakuomba tafadhali, nimekosea, NISAMEHE πŸ’”πŸ˜­πŸ˜­πŸ˜­.”

NAAAAM HUU NDIOOO MWISHO WA SEASON TWO

Share kwa ndugu na marafiki

WhatsApp
Facebook
Twitter

Chagua kipande kinachofuata

UTAMU WA JAMILA FULL

SHEM MI NATAKA FULL

TOBO LA PANYA FULL