LOML | Love Of My Life (119)

𝐋𝐎𝐌𝐋 (𝑳𝒐𝒗𝒆 𝒐𝒇 𝒎𝒚 𝒍𝒊𝒇𝒆) ❣️:119
Kaka nisikilize, ukiwa karibu na Mungu wewe na familia yako na yeye atakuwa karibu nanyi. Trust me ninachokueleza No prayer goes in Vain(Hakuna maombi huenda bure) kila ukiomba Mungu anafanya namna. Nakuomba Kaka.”

Nilimtazama tu, na wakati huo simu yangu ilikuwa inaita. Nilipo tazama alikuwa ni baba yangu. Nilishusha pumzi, na kusema “baba tena.”


Willy aliniambia “pokea kaka pengine kuna tatizo.”
Nilipokea simu ya baba yangu, nilipoitq tu “baba!!”
Baba yangu aliniuliza “upo wapi?”
Nilimwambia kwa upole “nipo na rafiki yangu baba, kuna tatizo?”

Baba aliniambia “Tatizo lipo, mkeo ametaka kujiua huko kwao, na unatafutwa hupatikani hivi kijana wangu una shida gani?”
Nilishtuka na kusema “baba unasemaje?, kujiua kivipi, una maana gani?”

Baba yangu aliniambia “alikunywa vidonge vingi kwa wakati mmoja, muda huu ninavyo zungumza tupo hospitali. Fanya haraka Njoo hapa.”
Nilichoka, hata kutoa machozi mimi nilichoka. Nilipokata simu nilisema “Gabriella alitaka kujiua wapo hospitali.”

Kaka Willy alishangaa na kusema “Mungu wangu balaa gani hili, anaendeleaje?”
Nilimtazama kaka Willy nikisema “sijui hata nilikosa wapi, baba anasema wanaendelea vizuri Ila wapo hospitali.”
Willy alinitazama na kusema “tuondoke, fanya tuondoke.”

Safari hii hata kubisha sikuweza, niliingia ndani ya gari na kuondoka na safari ilikuwa ni kwenda hospitali. Nilipofika pale mama yake Gabriella aliponiona tu alilia kwa uchungu akisema “alitaka kufa mwanangu, alitaka kujiua. Tafadhali yamalizeni mwanangu nakuomba.”

Nilimtazama baba, na baba yake Gabriella walikuwa wamechoka wananitazama tu. Nilimkumbatia huyu mama ajisikie vizuri. Baada ya hapo niliuliza “mke wangu yupo wapi?”
Mama alisema “amepewa dawa ili apumzike. Sidhani kama unaweza kumuona.”

Share kwa ndugu na marafiki

WhatsApp
Facebook
Twitter

Chagua kipande kinachofuata