LOML | Love Of My Life (12)

π‹πŽπŒπ‹ (𝑳𝒐𝒗𝒆 𝒐𝒇 π’Žπ’š π’π’Šπ’‡π’†) ❣️:12
Tunapanga vitu huku yeye na simu, akimaliza anaweka pembeni kidogo inaita mpaka nachukia sasa niliamua nijikaze kama alivyosema wapo kwenye matatizo. Dereva alipiga simu kuwa amefika, nilimuelekeza afuate mizigo na kisha tuendelee na safari. Unajua tangu tunaingia ndani ya gari, mpaka tunafika nyumbani mke wangu na simu tu. Sikupenda kabisa hii tabia. Lakini nitafanyaje na nimeambiwa tayari kuwa ana matatizo.

Nilishuka na mke wangu, kama ambavyo ipo nyumba ni mpya lakini kila kitu kipo vizuri kabisa. Madam ambaye tumeandaliwa pale nyumbani alitupokea. Niliingia ndani na mke wangu.

Hakuoga hata zaidi alibadilisha nguo tu, alinibusu huku anaongea na simu na kuondoka zake. Nilibaki nina mshangaa tu mke wangu.

Nilipokuwa chumbani nilipata wazo nimpigie simu mama yangu, nilimpigia mama, mama alipokea na alisema β€œhutajwi mwanangu, tumetoka kuzunguma kuhusu wewe sio muda hapa, eenh niambie safari muda gani?”

Nilitabasamu na kisha nilimwambia β€œndiyo maana nimepiga nikujulishe kuwa hatujasafiri kuna changamoto kidogo.”
Mama alishangaa na kuuliza β€œnini tena?”

Nilielezea kwa udogo tu na mama alisema β€œooh jamani, Mungu awasaidie sana, naimani litapita tu.”

Nilisema kwa upole β€œhata mimi naamini hivyo mama, basi mimi napumzika kidogo tutawasiliana wakati mwingine, msalimie baba.”

Mama aliniambia β€œamekaa hapa anakusikia, amekukumbuka tu.”
Nikacheka na kusema β€œnawapenda wote.”
Tukacheka.

Nilijilaza kitandani, ile nafumba tu macho yangu. Yule binti huyu hapa, ninamuona kila mahali, naona kabisa amechukua moyo wangu, akili yangu, mawazo ana miliki mpaka usingizi wangu.

Nilifumbua macho na kusema β€œNi nini hiki, kwanini nakuwa hivi?”
Kabla sijajijibu simu yangu iliita. Niliitazama kwa muda na kutabasamu, alikuwa ni rafiki yangu. Nilipokea simu hii na kusema β€œkaka!!”

Share kwa ndugu na marafiki

WhatsApp
Facebook
Twitter

Chagua kipande kinachofuata