
LOML | Love Of My Life (121)


๐๐๐๐ (๐ณ๐๐๐ ๐๐ ๐๐ ๐๐๐๐) โฃ๏ธ:121
Nikiwa nimekumbatiana na Giana kwa uchungu sana. Nilimuachia na kuanza safari ya kutoka nje bila kujali mtu yeyote. Nilitoka, nilitoka na hata rafiki yangu alinikimbilia nilimwambia โnisamehe rafiki yangu, naomba Niache mwenyewe kwasasa. Nataka kuwa peke yangu tafadhali.โ
Aliniambia kwa upole โMuda umeenda sana sasa, ni saa 2 na haupo vizuri Naomba nikuendeshe.โ
Nilimtazama na kusema โAsante sana, nashukuru sana.Lakini nakuomba Niache tafadhali.โ
Willy alinitazama tu na nikamwambia โNo prayer goes in Vain. Nataka kuongea na Mungu peke yake sasa hivi, yeye ndiyo atanipa majibu ya matatizo yangu yote. Nimechoka sana.โ
Sikutaka hata jibu lake niliingia ndani ya gari na kuondoka zangu, naelekea wapi, mimi sasa nilikuwa naelekea kanisani roho yangu ilikuwa inaniambia niingie kanisani nikakae tu hapo. Niliendesha gari kwa Muda kidogo na nilifika.
Baada ya kufika nilishuka, na wakati huo nashuka naona Pina ndiyo anaondoka. Nilijikuta namkimbilia. Nilipo mkaribia niliita โPina!!!!โ
Alisimama na kuitikia kwa kutaja jina langu โRodricky!!โ
Nilishusha pumzi, na Kisha Pina alisema โUwe na jioni njema Rodricky.โ
Nilimwambia kwa upole โtafadhali naweza kuzungumza na wewe?โ
Pina aliniambia kwa upole โnilikuambia ukae mbali na mimi, nilikuambia hivyo ina maana hukumbuki?โ
Nilivuta pumzi na kusema โwewe peke yako ndiyo unanielewa Pina. Nakuomba.โ
Pina aliniambia โnipo na bibi yangu, nitamchelewesha.โ
Nilimtazama na kusema โbibi namchukilia pikipiki, Kisha wewe nitakupeleka nakuomba.โ
Pina alisimama akinitazama na najua wazi haoni alisema โhaiwezekani.โ
Alishikana mikono na bibi yake, nilijikuta kwa uchungu nasema โPina amekunywa sumu, alitaka kujiua Kwasababu sijaweza kumsamehe.โ
Halafu Nilishindwa kujizuia kuumia kabisa. Pina alisimama, Kisha niliona ananizungumza na bibi yake, halafu bibi alianza kuondoka na yeye alipiga hatua kunifuata. Nilisogea pia na kusema โNimechoka Pina!!, Nimechoka sana.โ