LOML | Love Of My Life (133)

𝐋𝐎𝐌𝐋 (𝑳𝒐𝒗𝒆 𝒐𝒇 𝒎𝒚 𝒍𝒊𝒇𝒆) ❣️:133
Nilijitumia ushahidi kwangu, nikaweka tena simu ile mfukoni na sasa nikawa nainuka nashindwa nakaa. Nilitoa simu yangu tena nilimpigia Pina walau nipate msaada hakuwa anapokea simu yangu kabisa.

Ilinibidi nijikaze hapo natokwa jasho sana. Nilikuwa ninahisi moyo unataka kunitoka maana mapigo yangu ya moyo hayakuwa kawaida mpaak mishipa ya kichwa inanicheza.

Nilimpigia simu rafiki yangu Willy, na yeye pia alikuwa hapokei simu. Niliona nakosa msaada kabisa. Natakiwa kujikaza niinuke mpaka kwenye gari.

Sikuweza kabisa, nilianza kuona kama kanisa linazunguruka. Niliona kama viti vya kanisani vinazunguka. Kıla kiti kinazunguka. Nilishindwa kujipambania kabisa. Ni wazi nilianguka hapa na nilijikuta hospitali.

Nilikuwa sina nguvu, nimechoka na namuona dokta ambaye namfahamu. Nilichoka sana. Nikamuuliza “Dokta nimefikaje hapa?”
Alinigeukia na kutabasamu akisema “kaka unaendeleaje?”
Nilimtazama nikisema “nipo vizuri kabisa.”

Dokta aliniambia “ondoa shaka, rafiki yako alikuleta hapa na ulikuwa dispensary fulani sijajua ipi rafiki yako ana maelekezo yote Ila ndiyo alikuleta hapa ukiwa na hali sio nzuri kabisa.”

Nilishusha pumzi na kusema “yupo wapi?, tafadhali Naomba niitie.”
Dokta alinitazama na kusema “unatakiwa kutulia hapa, hali yako bado sio nzuri kabisa, naomba utulivu.”

Share kwa ndugu na marafiki

WhatsApp
Facebook
Twitter

Chagua kipande kinachofuata