LOML | Love Of My Life (138)

๐‹๐Ž๐Œ๐‹ (๐‘ณ๐’๐’—๐’† ๐’๐’‡ ๐’Ž๐’š ๐’๐’Š๐’‡๐’†) โฃ๏ธ:138
Nilikuwa najisikia vibaya sana lakini Pina alikuwa hapa ananilisha hata nilijikaza kunywa Supu. Ingawa sikumaliza ila nilipambana sana kunywa. Baada ya hapo nilishukuru nikisema โ€œnashukuru sana, Ubarikiwe sana Pina.โ€

Pina alitabasamu na kusema โ€œunatakiwa kujikaza na ule vizuri ndiyo utapata nguvu ya kuinuka hapa.โ€

Willy yeye alitoa vyombo na kisha alisema โ€œPina, mimi nakuacha. Inabidi nifike nyumbani. Sasa sijui una haraka sana ili baadaye nikurudishe nyumbani au sasa hivi?โ€

Pina alikuwa ameshika mkono wangu, mimi wakati nataka kujibu yeye alisema โ€œnitabaki hapa na Ricky, nitakuwa naye hapa. Usijali.โ€

Nilijikuta natabasamu hata Willy, alinitazama na kuniuliza kwa kuchezesha midomo โ€œni nani?โ€
Nilitabasamu tu, kisha Willy aliaga akisema โ€œbaadaye ndugu zangu. Kukiwa na tatizo nipigieni nitakuwa hapa haraka sana.โ€

Kwa kutania nilisema โ€œhata usiporudi.โ€
Wote tukacheka huku Willy akisema โ€œsasa hivi eenh, Pina ataondoka huyo utanihitaji.โ€
Tulicheka sana ingawa mimi cheko langu ni mdogo mdogo ila nilionekana kuwa na furaha hata kama naumwa.

Nilimtazama usoni Pina nikiwa nimelala pale kitandani, nikashika mikono yake na kusema โ€œthanks for coming, nilitamani sana kupata muda na wewe.โ€

Pina aliniambia kwa upole โ€œnisamehe sana kwa tabia yangu mbaya nimekuonesha.Kama kitu kibaya kingekutokea ningeshindwa kabisa kujisamehe. Nisamehe sana Ricky, nisamehe sana. โ€œ

Nilimtazama na kusema โ€œnakuelewa Pina, huna sababu ya kuomba msamaha na upo hapa. Asante kwa ukarimu wako. Nashukuru sana.โ€

Alitabasamu akaniuliza โ€œunajisikiaje?โ€
Nilimtazama nikisema โ€œnimechoka sana, hutojali kama nitalala si ndiyo?โ€
Alitabasamu na kuniambia โ€œmimi nipo hapa, nitakulinda, sitaondoka.โ€

Share kwa ndugu na marafiki

WhatsApp
Facebook
Twitter

Chagua kipande kinachofuata

KIBOKO YANGU FULL

CONNECTION YA BALTASAR FULL

CHAGUO LA MOYO FULL