
LOML | Love Of My Life (139)


𝐋𝐎𝐌𝐋 (𝑳𝒐𝒗𝒆 𝒐𝒇 𝒎𝒚 𝒍𝒊𝒇𝒆) ❣️:139
Nilitabasamu na kusema “usiniache peke yangu tafadhali, nakuomba sana.”
Pina alikuwa anazungumza kwa upole sana, alisema “nipo hapa, usijali, nipo hapa na wewe.”
Ni wazi dawa ndiyo zilizokuwa zinanichosha, nilikuwa nalala sana, kiasi kwamba nikilala mpaka naamshwa. Hivyo niliamshwa na Pina mchana huu, tena aliniamsha kwa upole sana akiita “Ricky!!, Ricky!!, Ricky amka sasa.”
Niliamka na kusema “ina maana nimelala sana?”
Pina aliniambia “sana, unatokwa jasho sana, unajisikiaje?”
Nilishusha pumzi nikisema “sijui Pina!!, Sijui!!”
Pina alisema “presha yako imeshuka sana, nilikuwa na daktari. Willy, mwambie tafadhali, chochote anawaza aachane nacho kwasasa kuna watu tunampenda na tuna muhitaji.”
Willy alisema “kama mimi Pina namuhitaji sana.”
Nilitabasamu na kusema “nitakuwa sawa, nitakuwa sawa ndugu zangu. Kaka Umerudi saa ngapi?”
Willy alitabasamu na kusema “ilikuwa lazima nilete chakula. Shemeji yako amepika.”
Nilitabasamu na kusema “nashukuru sana kaka, nashukuru.”
Willy alitabasamu na kusema “anakusalimu sana, ila nilimwambia ukiwa sawa ndiyo mtaonana.”
Nilimtazama na kusema “umefanya sahihi kabisa, nashukuru sana.”
Willy aliniambia “nilikuwa naongea na Pina, kasema bado atakuwa hapa na wewe leo. Hivyo mimi nawaacha mara moja nitarudi tena.”
Nilitabasamu na kusema “Pina, ubarikiwe sana. Nashukuru kwa kuacha kazi zako kwaajili yangu.”
Nilitabasamu, na kisha Pina alitabasamu. Na niliagana na rafiki yangu na alipoondoka nilimtazama Pina na kusema “Siku ya pili nilipokuona kuna maombi mazuri sana uliomba. Nayapenda sana. Natamani tufanye hapa pamoja.”
Pina alitabasamu, na kusema “Ni mengi sana, kila nikijisikia kuongea na Mungu naongea naye, unataka yapi?”
Nilimtazama na kusema “Mungu baba yangu, umenibariki na vitu vingi,,,, sikumbuki kıla kitu ila kuna vitu nakumbuka. Ilikuwa nzuri sana.”