LOML | Love Of My Life (143)

𝐋𝐎𝐌𝐋 (𝑳𝒐𝒗𝒆 𝒐𝒇 𝒎𝒚 𝒍𝒊𝒇𝒆) ❣️:143
Muda mwingi tulipenda sana kuwasiliana, mambo ya hapa na pale na nilikuwa nafurahia. Siku moja usiku wakati tunawasiliana alimpost mtoto wa miaka mitatu au minne status na alikuwa akimtakia siku yake ya kuzaliwa.

Niliona pia na kumuuliza “mtoto wetu, na mbona hunambii kama Tuna mtoto.”
Isack alicheka na kuniambia “inabidi tuzae mimi na wewe sasa huyu ni wakaka na wewe ukileta wako mambo yanakuwa safi kabisa.”

Nilicheka na kusema “nilijua huyu wangu Kumbe inatakiwa nifanye kazi.”
Tulicheka sana. Na hii siku ilipita tukiwa tumecheka na kufurahi sana.

Maisha yetu hayakuwa mabaya kusema kweli, Isack alikuwa akiniambia mambo mengi kwa uwaze kabisa mpaka miezi kadhaa mbele nilipokuja kugundua kuwa nina mimba, mimba ya Isack.

Nilimtafuta kwa upendo kabisa, na nilimuomba aje nyumbani kwangu tuzungumze. Wala hakuwa na tatizo, alikuja mpaka nyumbani na nilimuelezea hali yangu.

Isack alifurahi sana, alinikumbatia, alinibusu na kufanya nicheke tu. Nilimshukuru sana, nilimwambia “umenifurahisha sana, nilikuwa naogopa sana nikidhani utanikimbia.”

Alicheka na kusema “mimi, nikimbie hapana haiwezekani kabisa. Pina utakubali nikuoe?”
Nilizidi kushangaa sana, Nilitabasamu nikisema “nipo tayari, muda wowote mpenzi.”
Alifurahia na kunikumbatia kwa nguvu sana.

Mpaka anaondoka pale kıla kitu kilikuwa sawa na muda mwingi sana tulikuwa tunawasiliana kwa upendo kuhusu mtoto wetu anayekuja. Baada ya siku tatu aliniambia “baby, Nimeongea na familia yangu. Wanataka kukuona.”

Nilifurahi nikisema “unasema kweli mpenzi?”
Mpenzi wangu alicheka na kusema “jiandae, pendeza nakuja kukufuata kesho si huendi kazini kesho?”
Nilitabasamu nikisema “Yes Baby, kesho nipo off.”

Başı aliniambia “kama unahitaji chochote ili kesho upendeze utaniambia.”
Nitataka nini mimi, mimi nilikuwa na furaha tu. Nilikuwa nimefurahi sana.

Share kwa ndugu na marafiki

WhatsApp
Facebook
Twitter

Chagua kipande kinachofuata