
LOML | Love Of My Life (146)

𝐋𝐎𝐌𝐋 (𝑳𝒐𝒗𝒆 𝒐𝒇 𝒎𝒚 𝒍𝒊𝒇𝒆) ❣️:146
Isack alisema “lakini mama walau tupate hata chakula pamoja.”
Mama alisema “Nimekula tangu nazaliwa mwanangu, leo nimechoka.”
Mpaka hapa nipo tu nashangaa maana naona mama ana gübu na naona kabisa sitawezana. Mama aliondoka zake na kuniacha, mimi nilimtazama Isack na kusema “naweza kuondoka hapa tafadhali.”
Isack alisema “walau usubiri tupate chakula kwanza.”
Nilimuuliza kwa kumtazama “kwa raha gani Isack, kwa huo uongo ulionidanganya ilihali nilikuuliza kwa upendo kabisa.”
Alinitazama na kutaka kuzungumza na mimi, ila nilitoka bila hata kujali, nilikuwa naumia sana na vile wamenipokea ni tafsiri yake kuwa hawanipendi kabisa. Roho yangu iliniuma hata machozi nilishindwa kuzuia ukizingatia ninaye mtoto tumboni.
Isack alinifuata mbiombio, na aliniambia kwa huruma “Mpenzi wangu, nisamehe sana unajua Nakupenda sana. Nilihofia nikisema ungeweza kunikataa. Na ndiyo maana upo hapa, nataka kukuoa wewe na sio mwingine yeyote. Tafadhali huna sababu ya kuwa hivi.”
Nilimwambia kWa kulia “umenivunja sana moyo wangu, nilikuamini sana sasa kwanini umefanya jambo baya kama hili, kwanini?. Hata hivyo familia yako hawanipendi mimi, wala hawanitaki hata wewe umeona.”
Isack alinikumbatia akisema “sahau kuhusu mama, ndiyo yupo hivyo ila mkishazoeana utampenda mwenyewe. Ninaomba unisamehe kwanza tafadhali.”
Nilichukia sana, sikutaka hata kuongea naye zaidi nilimtaka anirudishe nyumbani mengine tutajua mbele ya safari.
Nilinuna wiki zima Isack ananibembeleza, lakini baadaye nilimsamehe na bado aliniambia Nia yake ya kutaka kunioa mimi.Sikuwa na shida kabisa nilikuwa nafurahia tatizo sikuwa najua nifanye nini ili kwao wanipokee mimi.
Nakumbuka, Isack na ndugu zake walienda mpaka nyumbani kwa bibi yangu lakini mama yake hakwenda. Hata nikamuuliza akasema kwa kutia huruma “kipenzi, mimi Nakupenda sana.

