LOML | Love Of My Life (149)

π‹πŽπŒπ‹ (𝑳𝒐𝒗𝒆 𝒐𝒇 π’Žπ’š π’π’Šπ’‡π’†) ❣️:149
Nikawa nawaza nimjibu nini bibi yangu, lakini kama bahati hivi mlango uligongwa. Kushtuka na kwenda kufunga alikuwa ni mtoto wa jirani anaomba beseni La kufulia.

Nilikaa kitandani nawaza sana naona kama ndoto zina maana na napuuza, wakati nawaza bibi yangu alinipigia.

Haraka nilipokea na bibi yangu aliniambia kwa upole β€œhujambo mjukuu wangu, una muda lini nataka kuzungumza na wewe.”
Nikamuuliza bibi yangu β€œkwema bibi yangu?”

Bibi aliniambia kwa upole β€œkwema kabisa na mbona hujaenda kanisani.”
Nikamjibu bibi kwa upole β€œnilichoka sana bibi, nisamehe tu. Najiandaa hapa nakuja sio muda unahitaji chochote?”

Bibi yangu aliniambia β€œnakuhitaji wewe mjukuu wangu.”
Nilicheka tu ila ndani ya moyo wangu nilipata hofu.

Nakumbuka nilikata simu Baada ya hapo Mimi nilijiandaa Kisha nilipita sokoni ndivyo nilivyo nikiwa naenda kwa bibi yangu au mtu wa karibu najua nitashinda huko basi nikanunua nyama, viungo na vitu vidogo vidogo nilivyo na uwezo navyo nikaenda mpaka kwa bibi yangu.

Niliwasiliana na mpenzi wangu na kumuelezea juu ya safari yangu na alikuwa pamoja na mimi.

Başı nilifika kwa bibi, tulipika, tulikula pamoja na tulipomaliza bibi yangu aliniambia β€œmjukuu wangu usiku nimeota ndoto hata sielewi.”
Nilimtazama na kuuliza β€œndoto Gani bibi?”

Bibi yangu aliniambia β€œnimeota unaolewa na Isack lakini gauni yako ya harusi ni fupiii sana, fupi hata huwezi kwenda kanisani wakati tulikuwa nayo ndefu tukawa tunajiuliza hata imekuaje.”

Nilishangaa na kusema β€œunajua bibi lazΔ±ma kuna kitu, hata mimi nimeota Mara shela jeusi, Mara shela limechakaa hata sijui ni kwanini. Nimeanza kuogopa bibi.”

Share kwa ndugu na marafiki

WhatsApp
Facebook
Twitter

Chagua kipande kinachofuata