LOML | Love Of My Life (153)

π‹πŽπŒπ‹ (𝑳𝒐𝒗𝒆 𝒐𝒇 π’Žπ’š π’π’Šπ’‡π’†) ❣️:153
Huyo Faraja sasa ndiyo mzazi mwenzake na mume wangu. Nilishangaa inakuaje wana ukaribu namna hiyo, alikuja pale na mama alisema β€œumemuona mke mwenzio sasa, sio mwenzako anakuja kwako kumuona mtoto au kuchukua mtoto unavimba. Umemkuta huyu, na ndiyo mwanamke wa kwanza wa Isack.”
Isack akasema β€œmama ni nini lakini?”

Mama alisema β€œkalete chakula binti yangu.”
Mimi hapo machozi yananitoka natamani kuinuka siwezi. Siwezi kwasababu mume wangu ananizuia. Machozi yanatamani kunitoka.

Başı huyo Faraja kaandaa chakula, nikawa kama nisile lakini mume wangu akawa ananishauri nile. Nikachukua tu kidogo hata mume wangu alisema β€œongeza chakula mke wangu.”

Nilimtazama na kusema β€œkinatosha mume wangu.”
Wifi yangu akasema β€œtangu lini bibi harusi akala sana mwisho anenepe vidole pete zisimtoshe.”

Halafu walicheka sana. Hata mume wangu alishindwa kuvumilia aliniinua akiwa amekasirika na tuliondoka huku mama akiita huku anacheka β€œwewe Isack, Isack Acha ujinga rudi hapa, wewe mpuuzi rudi nimesema.”

Mimi nilikuwa nalia tu namna wananikejeli. Hata mume wangu aliniambia β€œpole sana mke wangu, unatakiwa kujikaza.β€œ

Nilimtazama nikisema β€œkivipi Isack, hawanipendi, hawanitaki na inakuaje faraja yeye ndiyo yupo pale Ina maana ndiyo anapendwa sana una uhusiano naye gani?”

Mume wangu alikana, alisema uhusiano wao umeisha zamanΔ± na ndiyo maana amenioa mimi.Nilikuwa naendelea tu kulia. Roho yangu ilikuwa inaumia sana kusema kweli. Kukataliwa ukweni inauma sana, inatesa sana maana kuna watu wanatabia za kuumiza na kutesa sana.

Nilimwambia mume wangu β€œIsack Nakupenda sana, lakini kwa namna naona haya maisha Naomba niwe mbali na familia yako, sitaki kuwa karibu na familia yako kamwe.”

Share kwa ndugu na marafiki

WhatsApp
Facebook
Twitter

Chagua kipande kinachofuata

UTAMU WA JAMILA FULL

BIOLOGY TEACHER FULL

SHEMEJI UMECHOMEKA KWELI? FULL

KIAPO CHA MASIKINI FULL