LOML | Love Of My Life (167)

π‹πŽπŒπ‹ (𝑳𝒐𝒗𝒆 𝒐𝒇 π’Žπ’š π’π’Šπ’‡π’†) ❣️:167
Niliita β€œPina upo sawa?”
Pina alisogea kidogo, kisha alinifuata mpaka nilipo na alisema kwa upole β€œnisamehe sana kama nimekosea kwa mama na mkeo. Nilitaka ujisikie vizuri, nilitaka nimgawie mkeo maumivu yako, sikutaka akuumize tena na mimi nikiwepo. Nisamehe sana.”

Willy alishangaa, nilimtazama Willy na kusema β€œKaka unaweza kutuacha tafadhali.”
Willy alinitazama na kusema β€œbila shaka kaka.”
Aliinuka na kutoka zake.

Alipotoka nilipambana nikakaa, na yeye alinisaidia na kusema β€œHey my girl, napenda unavyonitetea, unavyo nipambania. Kusema kweli peke yangu bila wewe siwezi.

Umenipa nguvu ya kupambana, na kujiona nina thamani kubwa. Mimi najua uliyosema yote una maanisha Pina. Ina maana ulikuwa unatania kuwa unanipenda sana, utaniheshimu na kunijali sana.”

Pina alitabasamu na kisha alisema β€œRicky pleaseee!!”
Nilimvuta akae karibu yangu na nilimkumbatia na kusema β€œPleaseeeee!!, Pleaseeeeee!!, nakupenda.”

Akaniambia kwa upole β€œWapo sahihi, sikustahili, siendani na wewe, sivutii, sioni, maskini na bado ninaye mtoto, zaidi ya hayo yote nina maumivu makali.”

Nilisema kwa upole β€œPina mimi ndiyo sikustahili, siendani na wewe, sivutii, sioni na mimi ndiyo maskini kwasababu ni
Mjinga na mpumbavu niliacha mjinga kama yule atawale hisia zangu.”

Share kwa ndugu na marafiki

WhatsApp
Facebook
Twitter

Chagua kipande kinachofuata