LOML | Love Of My Life (172)

π‹πŽπŒπ‹ (𝑳𝒐𝒗𝒆 𝒐𝒇 π’Žπ’š π’π’Šπ’‡π’†) ❣️:172
Nilimtazama Willy na kusema β€œMoyo umechoka sana, Nipo hapa kwasababu ya mambo yake ya ajabu. Willy kwa alicho nifanyia hata mbinguni sidhani kama bado tupo kwa orodha ya wanandoa. Ndoa yetu imekufa kabisa.

Nikitoka hapa, kabla ya kwenda popote ni kanisani kufuatilia taraka. Tena natamani iwe haraka sana na nifanikiwe kwenye hili. Kusema ukweli sitamani hata kukumbuka mimi ni mume wake au nimewahi muoa. Ni mshenzi sana.”

Willy alishangaa na kuuliza β€œni serious namna hiyo?”
Nilisema kwa upole β€œnashangaa hata ujasiri huo ametoa wapi kuonekana na kujiliza kwangu. Alipaswa kuona aibu, na kujificha maisha yote. Kaka ipo siku nitakuelezea haya kwasasa acha nipumzike tu sitaki kuteseka lakini niambie vipi Pina?”

Willy alitabasamu na kusema β€œNimempenda.”
Nilimtazama na kusema β€œongea vizuri kaka, umempenda aje sasa shemeji yako yule.”

Willy alicheka akisema β€œumekamatika kaka, toto zuri lile aiseee, halafu haachi kunishangaza. Mmenipa raha sana.”
Nilitabasamu nikisema β€œnitumie ile video.”
Akacheka akisema β€œnilijua tu lazima, lazimaaa!!”

Tulicheka, na mwisho wa yote alinitumia video, akaniaga na kuondoka zake nilibaki chumbani peke yangu. Nilikuwa namuwaza tu Pina wangu, na kutabasamu hata nikapitiwa na usingizi.

Ulipita muda kidogo tu, baba yangu aliingia na aliniamsha. Nilipoamka baba yangu alinikumbatia kwa furaha sana na kusema β€œmwanangu una shida gani, unapata tatizo husemi mpaka unalazwa umenyamaza tu, au unatuchukia wazazi wako maana sijakuelewa. Hata mimi msiri wako, eenh kijana wangu. Unajua wazi mimi bila wewe sio kitu. Wewe ndiyo nguvu yangu na sasa unataka nife au wewe ufe nilie mpaka udongo unimeze na mimi.”

Share kwa ndugu na marafiki

WhatsApp
Facebook
Twitter

Chagua kipande kinachofuata