
LOML | Love Of My Life (176)

𝐋𝐎𝐌𝐋 (𝑳𝒐𝒗𝒆 𝒐𝒇 𝒎𝒚 𝒍𝒊𝒇𝒆) ❣️:176
Baba alitabasamu akinifuta machozi huku uso wake ukionekana kuumia akisema “mwanaume anajikaza, mwanaume anafanya maamuzi.Mwanaume yeyote yule ni mtu wa msimamo.
Usijali kuhusu mama yako, najua unaelewa wanawake walivyo but i promise you that, i will make her understands kila kinachoendelea. Najua kwasasa ni ngumu, wacha upone halafu mchakato wa taraka na nitakusaidia mwanangu.
Lakini sasa tuzungumze kuhusu huyu mwanamke mpya nataka kujua ni nani?, unampenda ?, wapi ametokea mbona ghafla hivi mwanangu..”
Nilitabasamu na kusema “baba she is very beutiful girl, ana moyo mzuri, ni rafiki yangu. Hatujafahamiana muda mrefu ila ananielewa kuliko mtu yeyote.
Ana mjua Mungu vizuri na msaada wake umechangia sana mimi kufika hapa leo hii. Ni mtu mzuri sana baba. Nilimuona mara ya kwanza siku ya ndoa yangu kanisani?”
Baba alisema “wacha weee, pale unakutana na soulmate ukishaoa.”
Nilicheka sana na kusema “kabisa baba , lakini niliheshimu ndoa yangu, kwasababu sikutaka kukuangusha.”
Baba alitabasamu na kusema “nakuelewa sana mwanangu, nakuelewa.”
Wakati tunazungumza mara mlango ulifunguliwa, alikuwa ni Pina amebeba kifungashio. Alikuwa anatabasamu na mimi nilikuwa natabasamu nikimwambia baba “ni yeye baba!!, ni yeye!!”

