LOML | Love Of My Life (202)

𝐋𝐎𝐌𝐋 (𝑳𝒐𝒗𝒆 𝒐𝒇 𝒎𝒚 𝒍𝒊𝒇𝒆) ❣️:202
Nilitabasamu na kusema “sana Pina, sana na pamependeza.”
Pina alitabasamu na kusema “waoooo!!, ni pazuri sana, eenh niambie pamendeza sana.”
Nilitabasamu na kusema “sana Mpenzi.”

Alianza kama kunipapasa, hapa ndiyo nikatoa fimbo ambayo nilikuwa nimeishikilia mimi na kusema “hii ndiyo zawadi yako.”

Nilimpatia mkononi na kusema “mimi nikiwepo huna sababu ya kutumia. Nikiwa mbali na wewe utatumia fimbo hii. Ni nzuri sana, Ina fanana sana na wewe, halafu Ina ng’ara vizuri sana.”

Pina ni kama sijui nimempa kitu gani kwa furaha ile. Alikuwa anaishika shika ile fimbo akisema “baby ni nzuri sana, tazama inavyo teleza. Ni nzuri sana yaani, nimefurahi sana.

Natamani uone namna nimefurahi Mungu wangu, Ricky umenikumbuka jamani. Sistahili this love, baby wewe ni mwanaume unayejali sana. Tazama, ona ilivyo nzuri.”

Nilimsogelea na kusema “nitafanya kila kitu kuhakikisha unakuwa na hii furaha maisha yako yote. Utakuwa na furaha hii hii. Karibu sana Pina.”

Pina alinikumbatia kwa nguvu, hata nilimbeba na kuanza kuzunguka naye, Kisha Tulijikuta tumeangukia kitandani. Alikuwa juu yangu, na mimi nilikuwa chini, nikawa namtazama namna alivyo mzuri, alikuwa ametulia tu.

Kisha nilimbusu taratibu midomo yake mizuri, alinibusu pia na Kisha tulijikuta tunacheka. Tulicheka huku Pina alisema “mimi ni mzito sana, nilisahau mgonjwa wangu hana nguvu kabisaa.”

Nilicheka nikisema “huna akili ujue, utakuja kuniua mimi.”

Share kwa ndugu na marafiki

WhatsApp
Facebook
Twitter

Chagua kipande kinachofuata