LOML | Love Of My Life (209)

𝐋𝐎𝐌𝐋 (𝑳𝒐𝒗𝒆 𝒐𝒇 𝒎𝒚 𝒍𝒊𝒇𝒆) ❣️:209
Alitabasamu na kusema “nashukuru sana shemeji.”
Aliingia ndani, nikamuuliza anachohitaji na mama Babuu alimuhudumia. Wakati anapata zake juisi nilimtazama na kusema “kwema shemeji, karibu.”

Alinitazama kWa upole na kusema “shemeji yangu, sijui kitu Gani kimetokea kwenu lakini nakuomba kwaajili ya maisha ya watoto na mimi mrudishe mume wangu kazini. Nimeumia kuona kuwa mume wangu hafanyi Tena kazi na wewe na hakuna sehemu anapata.

Shemeji maisha yamekuwa magumu sana kwetu. Nikaona nije hapa kwa niaba yake kuomba msamaha kwa maana hata sijui ni wapi amekosea.”

Maskini ya Mungu, mwanamke huyu angejua mume wake alichofanya kwa mke wangu. Mimi na yeye tumesalitiwa asingekuwa hapa kumuombea msamaha. Lakini kwakuwa hajui acha afanye wajibu wake kama Mke na mimi kutoka ndani ya moyo wangu ndoa yake hainihusu, Mungu peke yake ndiye atakayemnyoosha akae kwenye mstari.

Nilimtazama shemeji yangu nikamuuliza “unajua alichofanya?”
Shemeji yangu alinitazama na kusema “hapana shemeji, haniambii kitu chochote.”
Nikamuuliza tena “anajua kuwa upo hapa?”

Bado alinijibu “hapana, hajui chochote kile ni mimi tu nimeamua kujiongeza.”
Nilishusha pumzi na kusema kwa upole “shemeji yangu, siku nyingine usirudie kumuombea mtu msamaha kwa kosa ambalo hulijui kabisa.

Usibebe msalaba wa mtu ambaye amejitakia mwenyewe. Yeye mumeo anajua alichofanya kwangu, anaelewa kosa lake na hayupo tayari kutubu na badala yake yeye mwenyewe ameacha kazi. Mimi sijamfukuza kazi.

Lakini ukweli ni kuwa hata kama angebakia, kwa kitendo amenitende ni kuwa hastahili msamaha wangu. Ningemfukuza, amejiwahi.Na hata nikimsamehe hawezi kuwa karibu tena hata kuwa sehemu ya biashara yangu haiwezekani. Mungu atamsaidia atapata tu kazı mahali pengine. Na kuhusu wewe shemeji au watoto ukiona nafaaa kukusaidia kwa chochote nyumbani unapafahamu au kazini kwangu unapafahamu.”

Share kwa ndugu na marafiki

WhatsApp
Facebook
Twitter

Chagua kipande kinachofuata