
LOML | Love Of My Life (221)

๐๐๐๐ (๐ณ๐๐๐ ๐๐ ๐๐ ๐๐๐๐) โฃ๏ธ:221
Akiongea kizungu chake kwa upole sasa mimi natabasamu, nilimwambia โnipo hapa mama, unataka kusikia nini kutoka kwangu.โ
Pina aliniambia โsauti yako, sauti yako ni sababu ya maisha mapya kwangu, I love the way you talk, haswa ukisema nakupenda Pina wangu, nachanganyikiwa.โ
Nilitabasamu na kusema โNakupenda Pina wangu.โ
Akakaaa kimya, nikaita โPina!!, Pina!!, Pina unanisikia.โ
Akacheka na kusema โnilishachanganyikiwa uliposema Nakupenda Pina wangu.โ
Nikacheka nikisema โhivi unajua akili huna Pina.โ
Alinijibu kwa upole โkwaajili yako Ricky, kweli sina akili, Sina kabisa, crazy for you baby boy!!โ
Nilitabasamu na kusema โPina madeko wangu, napenda ukideka, unanikumbusha kuwa mimi ni mwanaume na natakiwa kukudekeza zaidi. Lakini sasa, ukisema Nakupenda Ricky wangu ndiyo nachanganyikiwa.โ
Alicheka na kusema โLoml, nakupenda sana.โ
Nilicheka nikisema โPina sitaki, Loml ni yangu, umeniibia, umeniibia ni yangu hiyo.โ
Pina alicheka akisema โuna hati miliki
Yake, ni yangu na nishasajili kabisa.โ
Hapo nishafika nyumbani tupo tunagombaniana Hati miliki ya LOML ni ya nani. Na wote mnajua ni yangu sema tu Pina ni mkorofi. Baลฤฑ tunacheka mpaka naingia sebuleni ni fujo. Nilimtazama Willy huku natabasamu nikasema โLOML.โ
Pina akasema โSitaki ni yangu mimi ndiyo nikuite hivyo.โ
Nikacheka na kusema โacha utoto Pina, ujue Willy yupo hapa anatuona hatuna akili. Nitakupigia sawa My Fortune.โ
Pina alisema โno no nooooo no no hii ndiyo naimiliki kabisa.โ

