
LOML | Love Of My Life (237)

๐๐๐๐ (๐ณ๐๐๐ ๐๐ ๐๐ ๐๐๐๐) โฃ๏ธ:237
Baba alinitazama na kusema โmwanangu najua mama yako amekukwaza msamehe si unajua mambo ya wakina mama.โ
Mama alinitazama na kusema โmwanangu ni kweli nilikuwa sitaki uachane na Gabby lakini Baada ya kujua lile sitaki kusikia hata. Lakini kusema kweli sijui kwanini huyu kipofu.โ
Nilichukia na kusema โbaba ongea na mke wako tafadhali. Hakuna kitu sipendi kama anavyo muita mpenzi wangu kipofu. Mama anaitwa Pina, ni mwanamke wangu, atakuwa binti yako. Utake au usitake unanielewa sijui.โ
Mama alisema โmume wangu unaona, mtoto amerogwa huyu. Hawezi kunijibu mimi hivyo. Labda niwe nimekufa vinginevyo hawezi kumuoa Yule binti kabisa yani.โ
Baba alimtazama mama na kusema โhuna aibu, una Salฤฑ nini. Mimi ni baba yake na Pina nimempokea ni binti yangu. Kama wewe hutaki mimi nitahakikisha hawa wawili wanakuwa pamoja. Unakuaje na roho mbaya hivyo huna huruma hata kwa mtoto wako.โ
Niliona tu watagombana hapa, nilitumia ustaarabu nikamwita mama babuuu, alikuja na alipofika nilimwambia โtafadhali waandalie baba na mama Chai.โ
Baba alisema โhapana mwanangu, tushakunywa.โ
Nilimtazama na kusema โsawa baba, mimi ndiyo nilikuwa najiandaa niende kazini tutaongozana au kama bado mpo nimwambie awaandalie chakula.โ
Baba alisema โsisi tunaondoka mwanangu. Nitakutafuta kuna jambo tuzungumze.โ
Nilitabasamu tu kwa uongo na kusema โSawa baba yangu.โ
Mama alinitazama na kusema โmwanangu, najua unakasirika. Sina maana mbaya mwanangu. Simaanishi kitu kimoja. Inanisumbua na nashindwa kabisa kujizuia. Nadhani unanielewa mwanangu. Sijui nitawezaje kukabiliana na hili. Yote kwa yote unajua tupo pamoja na nakutakia mambo mazuri.โ
Nilitabasamu na kusema โwewe ni mama yangu. Sijui unawaza nini kichwani Ila mimi najua una niombea Mara zote. Sitakulazimisha umpende Pina. Ninao uhakika kuwa yeye ni mwanamke wa maisha yangu.
Ni mwanamke mzuri kwangu. Nashukuru Mungu kwa hilo na namshukuru Mungu nimeondoka kwa Gabby. Tuanze maisha mapya sasa wazazi wangu. Nawapenda sana na Asanteni kwa kuja.โ
Mama alinikumbatia, nilikumbatiana naye na Kisha baba na yeye alinikumbatia na waliniaga. Niliwatazama tu na kutikisa tu kichwa changu maana hi wazazi wangu na wanavyobishana mpaka naona huruma tu maana Wangejua Pina anavyonipa mimi, sina hata habari ya kumuacha. Hapa nataka tu mambo ya taraka yapite kiasi ndiyo nianze kuwaza juu yangu na Pina wangu.
Mama na baba yangu Baada ya wao kuondoka, nilirudi haraka chumbani kwangu. Baada ya kufika chumbani nilikutana na Pina akiwa amekaa tu na hali ya huzuni. Niliita โPinaaa!!, Pina mpenzi upo sawa?โ

