LOML | Love Of My Life (41)

π‹πŽπŒπ‹ (𝑳𝒐𝒗𝒆 𝒐𝒇 π’Žπ’š π’π’Šπ’‡π’†) ❣️:41
Mume wangu, please am sorry, hii sio tabia yangu tafadhali nielewe.”

Ni kama alizidi kunitia hasira, nilifoka nikisema β€œhiki ndiyo ulitaka kuniambia, nataka kujua ni nini, imekuaje, kivipi na kwanini Mara ya mwisho ulinigeuzia kama ni kosa langu. Gabriella sina muda wa kukubembeleza.

Hii ndoa inakufa, hii ndoa itazama sasa hivi sijui hata kama unaelewa nini nazungumza. Machozi yako hayatasaidia kitu hapa. Na sasa ndiyo Nina majibu ya kwanini sikuridhishi, zile kelele, zile kelele hujawahi piga kwangu wewe ni mwanamke wa namna gani, wewe ni nani?”

Mke wangu huku analia alisema β€œuna niridhisha mume wangu, sana nafurahia sana.”
Nilimtazama na kutaka kuinuka pale maana ananikwaza hasemi chochote.

Wakati nainuka alinishika mguu wangu na kulia sana akisema β€œni zamanΔ± sana, ni zamanΔ± mume wangu. Sijawahi kufanya hivi tena Baada ya wewe kuja kwenye maisha yangu. Ni wewe umenibadilisha, nilikuwa naelekea pabaya sana.

Umenifanya mpya na umetengeneza maisha yangu, ni wewe Ricky. Kabla ya kuwa na wewe nilikuwa na mwanaume. Mwanaume Yule ndiye aliyenifundisha kila kitu, kila kitu hata pombe kali ni yeye.

Alikuwa ni katili sana kwangu, alikuwa ni drug dealer, alifanya kila kitu kibaya kwangu. Alinipiga pale nikiwa sielewi. Nilikuwa naishi kwa matakwa yake. Hakuna alichosema mimi nipinge. Alikuwa ana wivu sana, alikuwa anasema ananipenda sana.

Share kwa ndugu na marafiki

WhatsApp
Facebook
Twitter

Chagua kipande kinachofuata

SHEM MI NATAKA FULL

UTAMU WA JAMILA FULL

BINTI MDUNGUAJI FULL

UKO HOME NIJE FULL